Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

WEMA, IDRIS MAHABA NIUE!

WAANDISHI WETU
WAPENZI? Kwa mara nyingine Beautiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu amesababisha kichwa cha habari kufuatia kunaswa ‘live’ usiku mnene akiwa na mshindi wa Shindano la Big Brother Hotshots 2014, Idris Sultan wakioneshana vitendo vya ‘nakupenda tu’ mbele ya kadamnasi, Risasi Mchanganyiko lina mkanda kamili.
Beautiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu akiwa na mshindi wa Shindano la Big Brother Hotshots 2014, Idris Sultan.
NI ESCAPE ONE MIKOCHENI
Wawili hao walinaswa wakioneshana mahaba niue hayo usiku wa kuamkia Machi 29, mwaka huu kwenye Ukumbi wa Escape One, Mikocheni jijini Dar walipokuwa wamekwenda kushuhudia shoo kali ya mpambano kati ya Bendi za The African Stars ‘Twanga Pepeta’ na FM Academia ‘Wazee wa Ngwasuma’.PICHA LILIVYOANZA
Awali, paparazi wetu aliyeamua kulivalia njuga tukio hilo alimshuhudia Wema akiingia ukumbini humo akiwa sanjari na kampani yake, akiwemo shosti wake mkubwa kwa sasa, Aunt Ezekiel na mshauri wake  kikazi, Petit Man.
Walikwenda kukaa kwenye viti vilivyokaribiana na kuanza kufuatilia mpambano wa bendi hizo mbili kubwa nchini uliokuwa ukiendelea jukwaani kwa kishindo kikuu.
Idris akimweleza jambo Wema Sepetu.
PETIT AKAA NA MADAM
Kutokana na mpangilio wa watatu hao, Petit Man alikaa katikati ya Wema (kushoto kwake) na Aunt, lakini muda mwingi alikuwa akinong’onezana na Madam huyo huku wakionekana kuzungumza mawili matatu yahusuyo mpambano huo unavyoendelea.
IDRIS NDANI YA NYUMBA
Ndani ya dakika kama ishirini tangu Wema na msafara wake waingie ukumbini humo, Idris naye aliwasili akiwa ameongozana na mdogo wa hiari wa Wema aitwaye Bite pamoja na mtu mwingine ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja. Nao walikwenda walipokuwa wamekaa akina Wema.
ONA HII SASA
Kuonesha kwamba itifaki inazingatiwa, Idris alipofika mahali hapo, Petit alisogeza nyuma kiti chake na kuwafanya Wema na Idris waweze kukaribiana na kuzungumza kwa ujirani zaidi.
Wakipozi kimahaba.
WAANZA KUNONG’ONEZANA
WAFUTANA JASHO
Kama vile hiyo haitoshi, ilifika mahali Wema alionekana usoni kuvuja jasho kwa mbali, basi alichukua skafu ya Idris kutoka shingoni na kujifuta ambapo Idris naye alimsaidia na baadaye Wema naye alifanya vivyo hivyo pale mwenzake huyo naye alipotokwa na jasho.
Staa katika tasnia ya filamu Bongo, Wema Isaac Sepetu.
“Mh! Mwenzangu we acha tu. Hii ndiyo inaonesha sasa Wema na Idris kuna kitu, maana siku za hivi karibuni, kila alipokuwa anakwenda Wema, Idris naye alikuwa hakosi sasa leo hapa ndiyo full mahaba niue, hatari,” alisikika mpenda ‘ubuyu’ mmoja.
PICHA ZINAJIELEZA?
IDRIS AGOMA KUZUNGUMZA
Jitihada za kuzungumza na Idris ziligonga mwamba kutokana na staa huyo wa BBA aliyejinyakulia kitita cha dola za Kimarekani laki tatu (zaidi sh mil. 514) kutokuwa tayari kuzungumzia lolote kuhusiana na ukaribu wake na Wema ukumbini hapo.
 
Mshindi wa Shindano la Big Brother Hotshots 2014, Idris Sultan.
MUDA WA KUONDOKA WAFIKA, WAONDOKA PAMOJA
Wakati shoo ikielekea ukingoni, paparazi wetu aliwashuhudia wawili hao wakiongozana  katika msafara mmoja na Aunt, Petit na Bite ambapo walitokomea kusikojulikana.

AIBU KUBWA MREMBO ADAKWA KWA WIZI HOSPITALI!

 
MREMBO mmoja aliyejulikana kwa jina la Mariam Moshi (23), mkazi wa Mwananyamala Ujiji, aliponea chupuchupu kuuawa na wagonjwa wenye hasira kali waliolazwa katika Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar baada ya kudaiwa kuiba nguo. 
Mariam Moshi akihamaki baada ya kukamatwa na nguo anazodaiwa kuiba katika wodi ya wazazi Hospitalini Mwananyamala.
Walinzi wa hospitali hiyo walimuokoa mrembo huyo kwa kumnasua mikononi mwa wagonjwa hasa wajawazito walioenda kujifungua, waliodai kwamba Mariam aliingia katika wodi yao na kuwaibia.Tukio hilo lilitokea Machi 27, mwaka huu saa tisa alasiri, ambapo mama mmoja ndiye alishtuka kwa kuona amechukuliwa kitenge chake kipya.
Mama huyo alipobaini ameibiwa, alitoka nje na kuangaza macho huku na kule akiangalia alipoelekea Mariam aliyekuwa wodini kwao, ndipo alipomuona akiwa anatoka nje kulielekea geti ambapo aliwapigia kelele walinzi ili wamzuie.
 
Mariam akiwa mikononi mwa mlinzi wa hospitali hiyo.
“Walinzi walimsimamisha na kumuuliza kama aliiba kitu chochote wodini akirudishe, lakini alikataa katakata kuhusika ma wizi huo,” kilisema chanzo.
Hata hivyo, walinzi walipompekua, aligundulika kuwa na vitu alivyovifunga na kufunika kwa dera (gauni kubwa, refu alilokuwa amevaa).Askari wa kike walipomfunua gauni hilo, walimkuta akiwa na taulo ambalo alikuwa amelifunga kiunoni pamoja na kitenge alichokuwa akituhumiwa kukiiba wodini.
Baada ya wagonjwa kuona mali alizoiba mrembo huyo, ndipo akina mama wengine wakiwa na watoto wao walitoka wodini na kuanza kupiga makelele kwa hasira wakitaka apewe mkong’oto.
 
Walinzi hao wakitoa baadhi ya vitu alivyoiba.
Hata hivyo, walinzi wa hospitali hiyo walipoona Mariam amezongwa, ilibidi watumie nguvu kumuokoa na kumweka chini ya ulinzi wakisubiri namna ya kumpeleka polisi.Mariam alipohojiwa na waandishi wetu juu ya kitu kilichompeleka hospitalini hapo, alisema alikwenda kuwaona wagonjwa ambao hata hivyo alishindwa kuwataja. Alisema yeye ni mwenyeji wa Dodoma anayeishi Dar kwa kujitegemea.
Aliomba msamaha kwa kitendo alichokifanya, akisema kinatokana na maisha magumu na katika hali ya kushangaza zaidi, alipoulizwa kuhusu taulo alilokuwa amejifunga ndani ya dera alilovaa, alisema halikuwa la hospitalini hapo, bali aliliiba katika gesti aliyokuwa amelala siku hiyo.
 
...Wakimuhoji.
Wauguzi wa hospitali hiyo walidai malalamiko ya wagonjwa kuibiwa mali zao hospitalini hapo ni jambo la kawaida, hivyo siku hiyo ilikuwa ni ‘40’ ya Mariam.

PENNY: USISTA DUU UTATUMALIZA


ALIYEKUWA mtangazaji wa kituo cha redio cha Efm, Peniel Mungilwa ‘Penny’ amefunguka kuwa tabia ya baadhi ya wasichana mastaa kujiona masista duu itawamaliza kwa sababu watajikuta uzee unawakabili bila kuwa na ndoa.
Aliyekuwa mtangazaji wa kituo cha redio cha Efm, Peniel Mungilwa ‘Penny’.
Akizungumza na gazeti hili, Penny alisema mastaa wengi wanapenda kujiona ni matawi ya juu na kufikia hatua ya kudharau watu wengine kiasi kwamba hata wenye mapenzi ya dhati kwao hujikuta wakijiweka pembeni hivyo kuwafanya ‘kuchina’ wakati wakitafuta ndoa.
“Unajua kuna vitabia fulani hivi mastaa tunavyo, ya kisista duu ambayo inatufanya tuchine, maana wengi si wanatuogopa wakidhani sisi ni matawi ya juu wakati ni wa kawaida sana,” alisema Penny.

WASIKILIZE UHARIBU MAISHA YAKO

KUNA msemo mmoja mashuhuri sana unasema mswahili atakunyima kila kitu, lakini si maneno, ambao hapa tunaweza kuutafsiri kama umbeya. Yes, waswahili kwa umbeya hawajambo, wanazungumza mambo hadi mwenyewe unashangaa, yaani wanakufahamu kuliko unavyojifahamu mwenyewe, hata kama mmefahamiana muda mfupi tu uliopita.
Siyo jambo baya kwa sababu ndiyo utamaduni tuliorithi kutoka kwa vizazi vilivyotangulia na kadiri dunia inavyobadilika, ile hali ya watu kujali zaidi maisha yao binafsi kuliko ya mtu, ndivyo utamaduni huu nao unavyozidi kufifia.
Zamani ilikuwa kawaida kukuta kijiwe cha kahawa kinaanza asubuhi hadi usiku, siku hizi ni vijiwe vya kuhesabu na hata wanaokaa kutwa nzima kijiweni wanazidi kupungua, ingawa idadi kubwa ni watu wenye umri mkubwa. Vijana wanapungua vijiweni kwa sababu wameshagundua hakuna mtu wa kuwasaidia maisha yao pasipo wenyewe kwenda spidi.

Nina ushauri mmoja kwa akina dada kwa sababu wao ndiyo waathirika wakubwa wa umbeya. Hii ni kwa sababu akinababa kidogo wana nafuu. Wanasikiliza na kushiriki umbeya, lakini hawajali, yaani kwao mambo yanaishia hapohapo kijiweni, wachache wanaoweka kichwani, ni wale ambao fainali imeshawakuta!
Shiriki umbeya, kwa sababu wakati mwingine hauwezi kuukwepa, lakini kuwa na akili ya ziada. Siyo kila utakaloambiwa ni baya, hapana.
Yapo mengine ni mazuri, yaweke na yafanyie kazi, lakini nina uhakika, kwa asilimia zaidi ya 80, wanawake wanaongea mambo yasiyowasaidia, yaani huyu ana vile, yule ana hivi, wale wanafanya hivi na mambo mengine kama hayo.
Usiwasikilize na kuwaamini. Jione kama uko peke yako na kila anayekuzunguka ni adui. Kuwa makini na unachokiongea mbele yao, na usiwe wakala wa kusambaza kinachozungumzwa nao. Ukiwa hivi, utajiweka salama.
Na hata ukiletewa umbeya, kwamba unasemwa vibaya na huyu, usiwe na haraka ya kuamua mambo, wakati mwingine kusemwa vibaya na kuyaacha kama yalivyo ni baraka.Ila nikusisitize kitu kimoja, mwanamke ana nafasi kubwa zaidi ya kufanikiwa kimaisha duniani kuliko mwanaume, kwa sababu amepewa kila kitu, hasa uwezo wake wa kumshawishi mwanaume amsaidie kufikia ndoto zake!
KWAKO Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima. Pole sana kwa masaibu yaliyokupata na bila shaka, Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema, atakujaalia afya njema hivi karibuni.
Binafsi mimi mwananchi wa kawaida  nisiyekuwa na cheo chochote cha dini wala siasa, ni mzima wa afya na ninaendelea na shughuli zangu za kila siku likiwemo hili la kukuandikia wewe barua.
Kama ulikuwa hufahamu, kupitia hii barua yangu huwa nawakumbuka watu mbalimbali wenye majina katika jamii yetu. Leo nimekukumbuka wewe, japo naamini hatujawahi kuonana ana kwa ana lakini nautambua mchango wako kama kiongozi wa dini mwenye heshima kubwa kwa waumini wengi walio nyuma yako.
Wengi hawategemei kukuona katika jambo lolote ambalo litakuwa kinyume na matakwa ya Mungu. Mungu ni mpole na mnyenyekevu. Kwenye amri zake ametuzuia kufanya matendo maovu likiwemo la matusi.
Hapo ndipo kwenye msingi wa barua yangu. Kama msikilizaji mwingine, nilipata kusikia sauti yako ikimdhihaki kiongozi wa Kanisa Katoliki, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo kwa maneno machafu yasiyo na staha hata kidogo kutamkwa na kiongozi mkubwa wa dini kama wewe.
Nilijiuliza uliuweka uchungaji pembeni ulipokuwa unazungumza lugha kali kama ile? Maneno mazito kama yale hayakupaswa kuzungumzwa na mtu kama wewe, hata kama uliyekuwa unamtuhumu ametenda kosa kiasi gani, haikuwa busara hata kidogo kutamka maneno machafu yasiyo na hekima.
Maneno uliyoyatamka katika kinywa chako, yangetamkwa na mhuni wa mtaani wala nisingeshtuka. Nisingeona jambo hilo ni la ajabu kwani maneno kama hayo na mazito, yanatamkwa sana uswahilini kwetu.
Nimeshtuka sababu wewe ni mchunga kondoo wa Bwana. Wewe una dhamana ya kufundisha mema, ni kiongozi. Tena huongozi kikundi cha siasa, unaongoza kanisa lenye waumini wengi.Mbaya zaidi, kiongozi uliyemtusi naye ni kiongozi mkubwa wa dini. Ana dhamana kubwa ya kuwaongoza waumini kama wako au pengine zaidi yako.
Kimsingi busara zilipaswa kukuongoza kufikisha ujumbe uliokuwa umekusudia.
Kama uliona amekosea kutofautiana na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Baraza la Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (CPCT) na Jumuiya ya Kikristo (CCT) katika suala la Katiba Inayopendekezwa, ungetumia lugha nzuri kumueleza kwa hoja.

WAUMINI WA GWAJIMA WAFUNGA SIKU 40

WAKATI mambo yakiwa bado tete juu ya afya ya kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima la jijini Dar es Salaam, Mchungaji Josephat Gwajima, wafuasi wake wametangaza kufunga kwa muda wa siku 40 kuanzia juzi Jumatatu ili kuomba.
Mchungaji Josephat Gwajima akiwa hospitali.
Chanzo kilicho ndani ya kanisa hilo ambalo kwa sasa makao makuu yake yapo Kawe, kililiambia gazeti hili kuwa wafuasi hao wameamua kuliacha suala hilo mikononi mwa Mungu, hivyo wameona ni vyema kufunga kwa muda huo ili kumuombea kiongozi wao apate afya njema, lakini pia misukosuko inayomuandama imalizike.
“Jamaa wameona hali sasa inakuwa ngumu, wanafunga kwa vikundi, kila mmoja anamuombea apate afya njema baada ya kuzidiwa wakati akihojiwa, lakini pia wanataka haya mambo yamalizike, kwa hiyo wameona ni bora kumuachia Mwenyezi Mungu ili ayamalize,” kilisema chanzo hicho.

Waumini.
Mchungaji Gwajima alianguka ghafla wakati akihojiwa na maofisa wa Polisi wa Kanda Maalum ya Polisi Dar es Salaam, kufuatia maneno yake ya kashfa dhidi ya Askofu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarb Kardinali Pengo.
Baada ya kuanguka, mchungaji huyo amekuwa akitibiwa katika Hospitali ya TMJ iliyopo Mikocheni ambako hali yake imeelezwa kuwa bado tete, huku kukiwa na taarifa za kukamatwa kwa watu 15 wanaodaiwa kupanga mipango ya kumtorosha kiongozi huyo wa kiroho kutoka mikononi mwa polisi wanaomlinda.

UNYAGO WA KICHINA NA WANAWAKE WA KISASA, BALAA TUPU

Kama kawa nimerudi tena nikiwa na hasira kama faru aliyejeruhiwa, nakuuliza hivi kwa nini lakini? Tabia hiyo ndo uliyofundwa mkoleni? Jamani kabila lako si ndiyo  mafundi wa kuwaweka ndani wanawari, mnafundishwa nini, kuogea machicha ya nazi?
Loh! Mwana mbona unatia aibu kabila lako? Unamuaibisha somo yako na kuonekana mafunzo yote aliyokupa ulipokuwa mkoleni kazi bure.Jamani hivi ewe mwana, kutulia kwako kuna nini? Nyumba yako ina moto kila kukicha kiguu na njia na kusababisha kulichafua kabila lako na kuonekana kama mtu akioa kabila hilo kauoa moto. Sifa nyingine mbaya kuongea kama umemeza kanda, jamani nani aliyekufunda mkoleni kwamba mwanamke anazungumza kuliko mwanaume? Wewe mtoto wa kike umeolewa lakini mtu akikuangalia ulivyo anajua wewe ni changudoa, jamani mbona aibu, natamani kulia na kujiuliza hawa masomo wa sasa ni wakosa haya wasiojua nini maana ya mafunzo ya kumuandaa mwanamke.
Haya hukushika mafunzo ya kuishi na mwanaume hata uanamke wako huujui?
Mungu wangu! Yote tisa kumi ingia kwenye kicheni pati za sasa uozo mtupu, mwanzo zilivyoanza kwa kweli zilikuwa zikizingatia maadili kwa mtu aliye ndani ya ndoa yake kumfunda mwari japo nayo haikutosha kwa vile mafunzo ya kumuandaa binti huchukua zaidi ya mwezi mmoja.
Lakini leo inatisha, mpaka kuna kipindi huwa namuomba Mungu atusamehe kwa vile uchafu tunaofanya kwenye kicheni pati zetu matokeo yake ndoa zimekuwa mnaoana asubuhi mnaachana jioni.Sasa hivi umekuwa unyago wa Kichina kila mtu ana ruksa kuingia na kusema, na anayeelezwa yanaingilia kulia yanatokea kushoto akitoka ana yake basi ndani ya nyumba balaa tupu. Jamani hii kali inafikia hatua eti watu wanamchukua shoga (mwanaume si riziki) kwenda kumfunda mwari, jamani hii ni laana au nini. Mbona tumekuwa tunautia najisi uanamke wetu.
Leo hii wanawake tumeshindwa kufundana wenyewe tunawaita mashoga. Hii si laana na kutufanya kila kukicha wanawake tupoteze maadili na nyumba zetu kuwa kama kaa la moto hazikaliki.
Hivi jamani huyo shoga anajua usafi wa mwanamke akiwa katika siku zake afanye nini? Kuna wanawake wengi leo hii hawajui wakiwa katika siku zao wafanye nini na uchafu wao wauhifadhi vipi. Sasa hivi kicheni pati imekuwa ndiyo sehemu ya watu kukaa utupu na kutukana kila neno baya kusemwa ndani ya kicheni pati.Kingine kinachochekesha ni pale unampa mtu asiyeijua ndoa kumfunda anayetaka kuolewa. Mtaani ana sifa mbaya kishata mtaa, yeye tambara la deki, yeye jamvi la wageni ndiyo unampa kipaza sauti amfunde muolewaji. Jamani eeh!  Usiyoionja huijui ladha yake, mwenye ndoa ndiye atakueleza ndoa ipo vipi.
Mwari ndoa ina mambo mengi ndoa bila uvumilivu hukai, haya huyo kishata mtaa atayajuaje kama siyo kuyasema asiyoyajua. Kuna ndoa leo hii ukiambiwa ina miaka hamsini lakini ndani yake kuna kila aina ya taabu na raha, maumivu na furaha lakini yote walivumiliana na kuwafanya wawe mfano bora wa kuigwa. Hebu mtu huyo asimame au akufunde kwa wakati wake utagundua vitu vingi ambavyo vitakufanya uijue ndoa kiundani. Jamani ukiingia ndani ya ndoa unatakiwa utulie ubadilike uonekane kweli mke wa mtu kwa tabia na mavazi yako. Tulia nyumbani msikilize mumeo toka kwa amri si kila kitu mtaani unakitaka wewe, sherehe gani ipite bila kwenda na kushona sare. Ukinyimwa unadai talaka, shuuutu mwari ndoa mbaya ukiwa nayo ikikutoka utaitafuta mpaka kwa waganga.
Hebu basi tutumie mafunzo ya unyagoni tuzilinde nyumba zetu pia tuufahamu uanamke wetu ili tufute ile dhana mbaya wanawake mwalimu wetu kipofu, kwa mambo yanayoendelea naona mwalimu wetu hana kichwa kabisa. Yangu nimemaliza.

Migomo yaendelea kutikisa kila kona nchini Tanzania ambapo Tabora wafanya biashara nao wagoma.

Wananchi manispaa ya Tabora wamekuwa katika wakati mgumu wa kununua bidhaa mbali mbali baada ya wafanyabiashara  wa maduka yote ya maeneo ya soko kuu mjini humo,  kufanya mgomo wa kushitukiza wakiishinikiza serikali kwa mambo matatu, ya kumpa dhamana mwenyekiti wao kitaifa,Bw.Johnson Minja,kuongezeka kwa kodi asilimia mia moja,na matumizi ya mashine za EFDS.
Wakiongea na ITV katika  sehemu za maduka hayo akiwemo Mwenyekiti wa wafanyabiashara hao wamesema kuwa, hali ambayo imewafanya kugoma ni kutokana na malalamiko yao kutosikilizwa kwa mda mrefu, pamoja na juhudi ambazo zimekuwa zikifanywa na viongozi wao jambo ambalo limekuwa ni kitendawili huku wakiongezewa kodi. 
 
Akizungumza na wafanyabiashara hao mwenyekiti wa kamati ya ukusanyaji wa kodi wilaya hiyo ya Tabora mjini, ambaye pia ni mkuu wa wilaya hiyo Bw.Suleimani Kumchaya,amewataka kutokuwa na maamuzi yanayoathiri jamii bali kufanya makubaliano yanayoleta maendeleo katika jamii,kuliko kuchukua hatua za maamuzi na za haraka.

Matusi na ngumi zatawala baraza la wawakilishi Zanzibar.

Wajumbe wa baraza la wawakilishi wameweka tofauti za seriklai ya kitaifa pembeni na kuanza kutupiana matusi na  kutishia kupigana hadharani ndani ya baraza baada ya mabishano kuhusu hoja ya vitambulisho vya Zanzibar.
Hali hiyo ambayo haijawahi kutokezea  ndani ya baraza hilo ilianza wakati wajumbe walipokuwa wakianza  kuchangia hoja hiyo binafsi ya mwakilshi wa CUF Mh. Hamad Masoud ambapo mwakishi wa CUF jimbo la magogoni Mh. Abdillahi Jihad ambaye pia ni waziri alipaonza kumshambulia wazir wa nchi tawala za mikoa na idara maalum  Mh. Haji Omar Kheir
 
Hapo ndipo sakata hilolilipoanza  ambapo  naibu  waziri amabye ni CCM Mh. Haji Gavu alipaona kukwaruzana kwamaneno na matusi dhidi ya mwakilishi wa CUF na kutaka kugeuza ukumbi huo kuwa wa masumbwi.
 
Pamoja na jitihada za spika Mh. Pandu Ameir Kificho kutaka kuwepo kwa amani na utaratibu hakiusaidii  lolote na fujo hizo zikageuka kwa wawakilishi wa CCM Mh. Hamza Hassan Juma na mwakilishi wa CUF Mh. Salum Nassor ambao mnao wataka kuzipiga na kutishiana kwenda nje.
 
Hili ni tukio la pili kutokea ndani ya mkutano huu wa baraza ambao wawakilishi wa CUF na CCM kuvutana na kubishana kwa maneno ya matusi na kejeli.

Mwanamuziki Suma Lee Akata Shauri Aamua Kuacha Mziki, Aagiza Nyimbo zake zifutwe na Redio Wasizipige Tena

Hit maker wa ‘Hakunaga’, Suma Lee amesema kuwa hatafanya tena muziki kwasababu ameachana kabisa na maisha hayo na ameamua kusomea dini ya kiislam

Suma ambaye alitengeneza pesa nyingi kupitia hit yake ya ‘Hakunaga’, amesema kuwa hana mpango wa kuzitoa nyimbo zake zilizoko studio ambazo hazijatoka.

“sifanyi tena muziki na nimeachana kabisa na maisha hayo, na nyimbo zote zilizobaki studio nimezisimamisha zisitoke baada ya kuzilipia, “ Alisema Suma.

“kuna wimbo mmoja nimefanya na Cp ambao ndio ulikuwa wa kurudisha kundi la Parklane, pia nimeuzuia, labda Cp auchukue yeye.Kilichobaki ni kuwaombea wazazi wetu waliotutangulia, wengine walikuwa hawataki tufanye kazi hizi, kwa kuwa hawapo na hakuna wakutukataza tena, bora tukae na kuwaombea.”

Baada ya Mahojiano, Gwajima Aachiwa kwa Dhamana, Kwenye Hii Kesi Nani Mlalamikaji ?

Taarifa zimeenea kuwa baada ya Kutoka hospitalini Gwajima alikwenda moja kwa moja Kituo cha polisi Ostabey kwa ajili ya kumaliza mahojiano yake na Polisi kuhusu kumtukana Askofu Pengo...Baada ya mahojiano Askofu Gwajima Ameachiwa Huru kwa Dhamana....

Najiuliza kwa Sauti:
Katika Hili Sakata ni Nani Mlalamikaji ? Wakati kila mkubwa akijidai hausiki kwenye sakata hili
Je Pengo Amemshitaki ?

Faraja Kota Nyalandu 'Sio Lazima Ujue Kila Kitu Kila Wakati na Hutokaa Ujue Kila Kitu Kila Wakati'

Sio wakati wote utakuwa na majibu. Sio wakati wote utajua kama unapatia au unakosea. Sio wakati wote utakuwa na uhakika. Ninachotaka kukuambia ni kuwa; it is okay. Si lazima ujue kila kitu kila wakati. Na hautokaa ujue kila kitu kila wakati (translation: don't be self-righteous). But it's okay. Tujue mipaka yetu, tujue uwezo wetu na tujue mapungufu yetu. Tujitambue. Tujikubali. Tuanze kujiboresha kuanzia hapo. But put your worries to rest because it's okay, we are human beings afterall...here is one of my favourite lines: Feel the fear and do it anyway! P. S 

Kutongoza Wanawake Walioolewa ni Rahisi Kuliko Wasioolewa..

Hili sasa halina mjadala au ubishi kuwa kumtongoza mke wa mtu ni rahisi sana kama kusukuma tairi katika mteremko wa mlima kitonga. Lakini ni ngumu mno kutongoza hawa wasichana wetu wa kiswaz wana mlolongo mrefu na usumbufu.

Kwanini hali hii?

Karibuni

ESTER: BABA MZAZI ALINIKATAZA KUIGIZA


LEO hii kwenye Live Chumba cha Habari ya Global Publishers tunaye msanii chipukizi wa filamu za Kibongo, Ester Kiama ambaye pia ni mjasiriamali anayejishughulisha na biashara mbalimbali ikiwemo ya kuuza mkaa, pikipiki na magari.
Msanii chipukizi wa filamu za Kibongo, Ester Kiama akisisitiza jambo.
Katika mahojiano na safu hii huku akirekodiwa na timu nzima ya Global TV Online , Ester alisema hapendi watu wamjue mpenzi wake kwani anaogopa kuibiwa na wasichana wa Dar es Salaam kwa hiyo hapendi kumtangaza kabisa.
Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano ambayo pia yanapatikana katika Kipindi cha Exclusive Interview kupitia tovuti ya www.globaltvtz.com kitakachorushwa leo.
Mwandishi: Nini kilikusukuma mpaka ukawa muigizaji?
Ester: Nilikuwa napenda sanaa tangu nikiwa mdogo na zamani nilishajaribu kutaka kuigiza enzi hizo za Kibakuli na Muhogo Mchungu, nikawa naenda kuangalia wanavyofanya mazoezi pale Magomeni (jijini Dar) lakini baba yangu hakupenda na walijaribu kuja kuniombea nianze na mimi kuigiza baba yangu akawatimua akasema hataki kusikia hata kidogo kwa hiyo nikashindwa kwa sababu wazazi wangu walikuwa wanataka nimalize shule kwanza.
Mwandishi:  Umecheza filamu ngapi mpaka sasa hivi na una filamu ngapi za kwako mwenyewe?
Ester: Nimecheza nyingi kama kumi na moja na filamu ambayo imenitambulisha ni ile ya Profesa ambayo iko mtaani sasa hivi, filamu ambayo nimecheza vizuri ambayo huwa sichoki kuiangalia ni filamu yangu mwenyewe inayoitwa Ngoma Ngumu.
Ester Kiama akipozi.
Mwandishi: Ulimfahamu vipi Dude?
Ester: Dude nilikutana naye kwenye filamu yangu ambayo nimeiongoza ya Ngoma Ngumu, nilimuita aje acheze kwa sababu nilivyosoma ile stori ya filamu nilihisi ile sehemu inamfaa, akaja nyumbani nikamuona na ndiyo tukaanzia hapo lakini mwisho wa siku nikaona anafaa kuwa rafiki kwa sababu aliniongoza katika hiyo filamu.
Mwandishi: Ukaribu wako na Dude ukoje?
Mwandishi: Unakabiliana vipi na maneno yanayosemwa kuwa wewe na Dude ni wapenzi?
Ester: Ni jambo gumu kidogo, na siyo kwangu au kwa mpenzi wangu lakini kwa upande wa Dude pia kwa sababu naye si ana mke kwa hiyo pia ni jambo gumu na watu kuelewa ni ngumu zaidi lakini mwisho wa siku mpenzi wangu ananielewa.
Mwandishi: Umeolewa au una mpenzi?
Ester: Sijaolewa lakini nina mpenzi, siwezi kumtaja kwa jina kwa sababu sipendi watu wamjue na ninaogopa kuibiwa na wasichana wa Dar es Salaam wanaiba sana wanaume za watu.

Nguvu na Ushawishi wa Lowassa Waongezeka Maradufu

*Tafiti Mpya Za Kitaalamu Zadhihirisha Uhalali wake Kisiasa

*Kauli ya Jk yaongezewa nguvu na Tafiti Mpya za PTT

*Kauli ya mjumbe kamati kuu Jerry Slaa Yampa majibu nape na January "Chama chetu lazima kipeleke bidhaa inayohitajika sokoni, inayouzika na inayokidhi haja ya mnunuaji"

*Tafiti zabainisha nguvu ya Wapinzani Wa Lowassa Pinda na Membe, washindwa kutumia System kumzima Lowassa Zaweka wazi ushawishi wa Lowassa Kwa Umma.

Taasisi isiyo ya kiserikali ya Positive Thinkers Tanzania imetoa ripoti yake ya utafiti kuhusu mwanasiasa anayekubalika zaidi na wananchi katika nafasi ya Rais ajaye, Lowassa aongoza na nafasi ya 2 imeenda kwa Dr. Wilbroad Slaa huku Mwigulu Nchemba aking'ara kama kijana aliyeongoza kwa kukubalika kwa kukamata namba 3.
Ifuatayo ni orodha ya wanasiasa waliongia 10 bora na asilimia ya kura walizopata.

1. Edward Lowassa 22.8%
2. Wilbroad Slaa 19.5%
3. Mwigulu Nchemba 10.6%
4. Ibrahim Lipumba 8.9%
5. John Magufuli 6.8
6. Zitto Kabwe 6.7 %
7. Bernard Membe 5.9%
8. Mizengo Pinda 3.2%
9. January Makamba 1.6%
10. Mark Mwandosya 1.2%

Tafiti hizi zimedhirisha nguvu na ushawishi aliyonayo Edward Ngoyayi Lowassa Kama Kiongozi Kwa Jamii na Umma Wa Tanzania kwa Kiwango Cha Asilimia Alichopata Lowassa Ni dhahiri Shahiri Uchaguzi Ukifanyika leo basi ana nafasi kubwa ya kushinda uchaguzi huo.

Hii ni Tofauti na Wagombea wengine ndani ya CCM ambao kama watapitishwa na chama, chama kitalazimika kutumia nguvu kubwa mno ili kupata ushindi na ushindi ambao unaweza ukawa wa asilimia moja tena baada ya uchaguzi kurudiwa ikiwa ni sehemu ya marudio baada ya round ya kwanza kuonekana kutofikia asilimia.
  Tafiti hizi zinaipa kauli ya Mh mwenyekiti na Rais wa tanzania Amiri jeshi mkuu nguvu kwani alisema " ikitokea kuna mtu ananguvu ya kutosha na mnamuona anafaa kuwa Rais basi msisite kumshauri agombee, eeh mshawishini tuuh" kwa muda wa week sasa makundi mbali mbali kada na rika mbali mbali kutoka katika kila kona ya tanzania yamekuwa yakijitokeza kwenda kumuomba Lowassa agombee urais.

Kwa Tafiti hizi watu watapata majibu ni nani anafaa na kwa nini mamia ya watanzania wanajitokeza kumshawishi Edward Lowassa Agombee,Alisema hivi karibuni mjumbe wa kamati kuu ndugu jerry silaaa Yakwamba " chama lazima kipeleke mgombea anayekubalika anayeuzika na anayeweza kukipa chama ushindi" kauli hii ilikuwa mwiba na jibu kwa nape aliyewahi kutoa kauli isiyo ya kiungwana kwa kusema chama hakiwezi kumpitisha mgombea asiyesafishika hata kwa dodoki.

Kauli hii inapingwa na takwimu za tafiti za kitaalamu kwamba Lowassa Ni sawa na kiatu kilichokwisha pakwa kiwi ni kazi ya chama kukibrush tuu" pia kauli hii ni jibu linalomjibu January makamba yakwamba Lowassa Alishapita umri wa kufanya siasa ya maigizo tafiti hizi zinaonyesha namna january anatakiwa kukuza siasa yake watanzania Wamfahamu zaidi na apate uhalali wa kisiasa.
 Alisema mama Sophia simba mjumbe wa kamati kuu Kumjibu januaru " kama unaona wenzio wanaigiza kwa kutoa pesa ili watu wawashawishi nawe toa pesa tuone kama kuna mtu atakuja kukushawishi"Pamoja na nguvu kubwa ya kibobezi inayotumiwa na wabobezi hawa wawili pinada na membe bado siasa yao imeonekana kukosa uhalali kwa watanzania tafiti za za kitaalamu mara kwa mara zimekuwa sio rafiki kwa pinda na membe kwa takwimu za tafiti kwa chama cha ccm kumpitisha membe au pinda ni sawa na kupeleka KOFIA YA POLICE DUKANI UKAIUZE Nguvu ya Mwigulu Lamerck Nchemba Imeonekana kuwa Kubwa Kuliko Hata Wabobezi hawa wawili wanaotumia ubobezi wao kupitia system ya serekali na dola kushinikiza makundi mbali mbali kuwaunga mkono.

Hivi karibuni kumekuwa na tabiya ya makundi mbali mbali yanayopewa na kupokea vitisho kutoka kwa wabobezi hawa wawili kwa kosa la kutumia uhuru wao na Dhamira yao njema ya kumshawishi edward atangaze nia na agombee urais.

UKIUWA KWA UPANGA NAWE UTAULIEA KWA UPANGA, TAFITI HIZI ZINAONYESHA SI RAHISI KUZUIYA MKUKI KWA SHUKA

MIMI ‘MTU WANGU MZUNGU’ NDIYO NINI SASA? - 2

Karibuni sana wasomaji wangu wapendwa katika safu hii maalum kwa ajili ya kuelekezana mambo mbalimbali yanayohusu maisha kwa ujumla hasa upande wa mapenzi kama siyo mahaba.Mfano wa mambo hayo ni namna wenza wanaoishi na ndugu au wazazi wao wanavyopaswa kuishi kwa hekima bila kuwakwaza.
Kujiepusha na kauli zisizofaa ambazo mara nyingi zimekuwa zikiharibu uhusiano wao, kujiweka katika mazingira ya usafi wa nyumba na mavazi.Mambo mengine ni kuwa waaminifu katika uhusiano wao kwa sababu wenza wakiwa na michepuko huweza kuleta maradhi ndani ikiwa ni pamoja na migogoro inayosababisha kuachana.
KWA NINI UZUNGU UAMBATANE NA USALITI?
Wiki iliyopita tuliishia kwenye neno hili; ni sababu mbaya sana kusema ‘mtu wangu Mzungu’. Kisa hakuchunguzi, hakufuatilii.
Wengi wanaotoa madai au sifa hizo ni wale wasio na uadilifu na siku zote watu wasio na uadilifu ndiyo wanafurahia sana maisha ya kutofuatiliwa.Ukimwona mtu anasema mtu wake ni Mzungu maana yake ana mambo yake mengi ya siri lakini hayafuatiliwi kiasi cha kuwa kukamatwa au kujulikana nyendo zake.
Hii sifa imeshamiri sana katika jamii ya ‘Kiswahili’. Lakini wewe msomaji wangu ambaye upo katika uhusiano, chukulia kwamba, una mwenza anakusaliti lakini wewe hujui kwa sababu hufuatilii na unaitwa Mzungu. Je, siku ukijua Uzungu utauonaje?
 DHANA MBAYA KUWA NZURI
Mambo ya kutofuatiliwa yanaambatana na mawazo ya ubaya kuwa mzuri. Kwa nini nasema hivi? Kuna watu wanadiriki kusema hadharani maneno haya:“Mimi bwana simu yangu mwenzangu hashiki kabisa. Mimi sishiki yake na yeye hashiki yangu.”Hawa wanaosema hivi ni wana ndoa zaidi. Wanamwagiana sifa kwa kila mmoja kutoshika simu ya mwenzake, kwamba ni sifa kwao.
Lakini kusema ule ukweli, hata wewe msomaji tafakari kwa makini sana ukitumia akili za ndani. Je, ni sawa kwa wanandoa kuogopana kwenye simu? Mna nini cha siri ambacho mwenzako hatakiwi kushika?
 
MZUNGU MWENYEWE SASA
Kama utamkuta Mzungu anayesifiwa kwa kutokuwa na tabia ya kufuatilia mambo ya watu, atakwambia sababu kubwa ni kuamini.Niliwahi kuzungumza na mtu (Mzungu) mmoja anaitwa Frank, alisema kuwa, kwa Wazungu mtu kufumaniwa ni nadra sana kwani walio wengi ni waaminifu.
Alisema Wazungu wanaofumaniwa historia zao zinaonesha kuwa, alishatoka Uzunguni na kwenda kuishi mbali na kujikuta akibeba tabia za ugenini.Kwa hiyo ninapenda kumalizia mada yangu leo kwa kusema kwamba, matumizi  ya neno ‘mi mtu wangu Mzungu’ yasiambatane na usaliti wowote. Wapo wenza ambao hawaaminiki si kwa sababu wasiowaamini wana tabia za wivu uliopitiliza, bali kwa sababu ya matukio mbalimbali ya usaliti ya hao wasioaminika!
KUNA HULKA YA USALITI
Mbaya zaidi ni pale baadhi ya wenza kuwa na hulka ya usaliti. Wapo ambao hata akinaswa akisaliti si dawa ya kuachana na tabia hiyo, hao ndiyo wale ambao hupenda kuwaita wenza wao Wazungu. Tujisahihishe kuhusu hilo.Huu mwisho wa makala hii, tuungane wiki ijayo katika makala nyingine.


PAUL MAKONDA, DK SLAA WAMJULIA HALI ASKOFU GWAJIMA

 
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Wilibroad Silaa (kushoto), akimjulia hali Askofu Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda akimjulia hali Askofu Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima aliyelazwa Hospitali ya TMJ kwa ajili ya matibabu baada ya kupata mshituko katika mahojiano na polisi akituhumiwa kutoa lugha isiyofaa kwa Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo.
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Wilibroad Silaa (kushoto), akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda walipokutana Hospitali ya TMJ walipofika kumjulia hali Askofu Gwajima.

Baada ya Kuhamia Nyumba Mpya, Diamond na Zari Roho Mkononi, Yabainiki Kwake ulinzi ni Sifuri, Mwenyewe Akiri Kuishi kwa Hofu

TAHADHARI ichukuliwe! Habari zikufikie kuwa, baada ya staa mkubwa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz‘ na mpenzi wake, Zarinah Hassani ‘Zari’, kuhamia kwenye mjengo wake mpya uliopo Madale jijini Dar, imebainika kuwa familia hiyo inaishi roho mkononi kufuatia ulinzi sifuri, jambo linalowafanya kuishi kwa hofu tupu

Kikizungumza kwa hofu juu ya familia hiyo, chanzo chetu makini kilipasha kwamba, pamoja na Diamond kutumia mamilioni ya fedha kujenga nyumba hiyo ya gharama kubwa, sasa changamoto imehamia kwenye ulinzi na usalama wao

“Jamani watu wanampongeza Diamond kwa kuhamia nyumba mpya lakini wale jamaa aisee wanapaswa kuombewa kila kukicha.

“Pamoja na kushusha mjengo wa maana bado changamoto ni juu ya ulinzi wao.

“Huwezi kuamini Diamond bado anaishi kizamani sana na sijui kwa nini anajiamini kiasi hicho wakati anajua wazi kuwa yeye ni staa wa Afrika na hapaswi kuishi kwa ulinzi hafifu.

MAENEO HATARISHI?

“Nasema hivi kwa sababu hata maeneo anayoishi ni hatari sana kwake hivyo anatakiwa kuwa na ulinzi mkali ili tu siku moja asije akafanyiwa kitu ambacho taifa likaingia kwenye hasara ya kumpoteza nyota mkubwa kama yeye.

“Nina uhakika asilimia mia moja Diamond hadi leo hajaanza hata kufanya process (taratibu) za kuchukua silaha (bastola).

“Mimi naijua vizuri Madale ni sehemu ambayo watu huwa wanavamiwa mara kwa mara na wanaishi kwa hofu kama Diamond anavyoishi.

HIKI NDICHO KINACHOMPONZA

“Kitu kingine kinachomponza Diamond ni ishu ya kuweka kila kitu kilichopo ndani kwake mitandaoni. Usione kila mtu anasifia lakini kuna wengine wanavitolea macho.

“Kwa mfano katupia picha za toilet (choo) ambacho kimepakwa dhahabu na kusema kimegharimu shilingi milioni 70.

“Hajakaa sawa akatupia picha za jikoni kwake kuna vitu vingi vya thamani kubwa kila mahali mpaka kwenye korido kuna flat screen (runinga). Huko si ni kuwakejeli watoto wa mbwa? Ni vizuri akaacha kufanya hivyo kwa sababu anawapa watu tamaa,” kilitiririka chanzo hicho.

ANA ULINZI GANI?

Juu ya ulinzi wa nyumbani kwa Diamond, chanzo hicho kilidai kwamba, mbali na baunsa anayewalinda aitwaye Mwarabu hakuna askari wa silaha anayelinda nyumbani hapo hivyo jamaa anatakiwa kufanya haraka kuajiri walinzi wenye silaha.


Baada ya habari hizo na uchunguzi wa kutosha, Ijumaa Wikienda lilimsaka Diamond a.k.a Dangote au Chibu ili kujua namna anavyoishi na jinsi anavyoimarisha ulinzi wake na familia kwa jumla.

Diamond, mbali na kukiri kuwa na hofu, alikuwa na haya ya kusema: “Suala la ulinzi wangu nalijua mwenyewe lakini zaidi watu wanatakiwa kujua mimi nipo na mlinzi na ninaendelea kuimarisha ulinzi wa nyumbani kwangu.

“Sidhani pia kama ni suala zuri sana kwa watu kujua siri za ulinzi wangu ila mambo mengi ya kujilinda niko kwenye michakato ya mwisho kukamilisha na soon (haraka) mambo yote yatakaa levo maana huwezi ukafanya kila jambo kwa wakati mmoja,” alisema Diamond huku akikubaliana na ushauri wa gazeti hili juu ya kuongeza ulinzi alionao wa baunsa.

ILIWAHI KUMTOKEA SUGU

Huko nyuma iliwahi kumtokea Mwanamuziki Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema) ambapo alikuwa amerejea kutoka nchini Uingereza.

Akiwa amepanga nyumba nzima maeneo ya Tegeta, Dar, Sugu alifanyiwa makala ya runingani na kuonesha vitu vya thamani vya nyumbani kwake.

Siku chache baada ya kipindi hicho kuruka runingani, jamaa huyo alivamiwa na kuporwa kila kitu lakini yeye hakudhurika.

Emmanuel Mbasha Afunguka sakata la Gwajima katika Twitter, Asema Hayuko Tayari Kurudiana na Mkewe

Katika Sakata linaloendelea sasa la Gwajima Kumtukana Askofu Pengo na la Kuzidiwa na Kukimbizwa Hospitalini akiwa mikononi mwa Polisi , Emmanuel Mbasha ambae inasemakana yeye na mkewe kuachana kuna mkono wa Gwajima ametoa maoni yake kuhusu Sakata la Askofu Huyo..
Jisomee Hapa Chini:

TAMKO LA MAASKOFU NA WACHUNGAJI KUTOKA MADHEHEBU MBALIMBALI JUU YA TUKIO LA ASKOFU GWAJIMA.

Sisi maaskofu na wachungaji kutoka makanisa mbalimbali tumeshtushwa na kusikitishwa kwa taarifa ya ugonjwa wa Askofu na mtumishi mwenzetu Josephat Gwajima ambaye tarehe 27/03/2015 alifika kituo cha polisi cha kati kuitikia wito wa polisi uliomtaka kwenda kujibu shutuma za kutumia lugha ya matusi kwa kardinali Pengo.
Maswali yetu makuu ni kitu gani kimempata mwenzetu? Tunajiuliza, je vyombo vya usalama vimekua sio sehemu salama kama zamani?
Tukiwa bado tunatafakari hill, tumeshtushwa tena baada ya kupata taarifa ya kuwa Wachungaji Wasaidizi wa Askofu Gwajima pamoja na walinzi wake waliokuwepo hospitalini hapo kwa ajili ya kumuuguza nao pia wamekamatwa kwa tuhuma za. kutaka kumtorosha Askofu Gwajima. 
Jambo hili linashangaza zaidi maana wachungaji wale wale waliokuwa naye akiwa mzima wa afya wakati anaelekea polisi ndio wale wale wanatuhumiwa kutaka kumtorosha akiwa mgonjwa.
Ni jambo la kushangaza na lisiloingia akilini kuwa wasaidizi hao wa Gwajima walitaka kumtorosha wakati Gwajima kama angekua na nia hiyo angekwisha fanya hivyo mana alikuwa na uwezo wa kutoroka alipokua Arusha kwenye kikao cha Maaskofu wakuu wa makanisa ya Kipentekoste ambao alipata taarifa za kuitwa Polisi.
Isitoshe Gwajima aliitija wito na kwenda polisi mwenyewe kwa miguu yake bila kushurutishwa, wala hakufikishwa polisi kwa nguvu.
Swali: Kama alikua anaona ugumu wa kutoroka wakati hakuna polisi anayemlinda na huku akiwa mwenye afya tele, itakuaje rahisi kutoroshwa leo akiwa mahututi na akiwa kwenye ulinzi mkali wa polisi?
Mbona hii inastaajabisha?
Jambo jingine linalotupa shida ni kuhusu mlalamikaji wa kesi hii inayomkabili Askofu Gwajima. Tumeelezwa na wasaidizi wa Askofu Gwajima kuwa pale polisi walielezwa kuwa aliyefungua kesi hii sio Pengo ila mtu mmoja aitwaye Aboubakar.
Kwa ufahamu wetu juu ya sheria unatutuma kuamini kuwa Aboubakar sio MTU sahihi wa kufungua kesi hiyo sababu hawezi kutuonyesha ameumizwa kiasi gani na matamshi ya Askofu Gwajima.
Isitoshe, Kardinali Pengo mwenyewe ametamka katika Ibada yake ya Jumapili hii ya tarehe 29/03/2015 kuwa amemsamehe Gwajima, yupi tena mwenye uchungu wa kumzidi Kardinali Pengo?
 RAI YETU:
Rai yetu ni kwamba, ni vizuri serikali pamoja na vyombo vyake vya usalama vikatumia weledi katika kushughulikia mambo ya kidini na viongozi wake kwani yanaweza kusababisha chuki dhidi ya serikali na pia kupelekea mpasuko mkubwa wa kidini katika jamii yetu iliyo na historia nzuri ya umoja na mshikamano na ushirikiano katika matukio yote ya kimaisha.
Tunaomba serikali isaidie kuondoa mkanganyiko huu na busara kubwa itumike ili kuepusha uvunjifu wa Amani katika jamii.
MAAMUZI YETU:
Jambo hili linazungumzika, maana hata hivyo tumeshaazimia kukutana na IGP ili kupata suluhisho juu ya jambo hili.
Kwa niaba ya maaskofu na wachungaji:
Mwenyekiti: Askofu Dr. Mgullu Kilimba
Katibu: Askofu Dr. Dramas Mukassa
Na mwandishi
F.A.K
30/03/2015
© Copyright BONGO HABARI
Back To Top