Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

WASIKILIZE UHARIBU MAISHA YAKO

KUNA msemo mmoja mashuhuri sana unasema mswahili atakunyima kila kitu, lakini si maneno, ambao hapa tunaweza kuutafsiri kama umbeya. Yes, waswahili kwa umbeya hawajambo, wanazungumza mambo hadi mwenyewe unashangaa, yaani wanakufahamu kuliko unavyojifahamu mwenyewe, hata kama mmefahamiana muda mfupi tu uliopita.
Siyo jambo baya kwa sababu ndiyo utamaduni tuliorithi kutoka kwa vizazi vilivyotangulia na kadiri dunia inavyobadilika, ile hali ya watu kujali zaidi maisha yao binafsi kuliko ya mtu, ndivyo utamaduni huu nao unavyozidi kufifia.
Zamani ilikuwa kawaida kukuta kijiwe cha kahawa kinaanza asubuhi hadi usiku, siku hizi ni vijiwe vya kuhesabu na hata wanaokaa kutwa nzima kijiweni wanazidi kupungua, ingawa idadi kubwa ni watu wenye umri mkubwa. Vijana wanapungua vijiweni kwa sababu wameshagundua hakuna mtu wa kuwasaidia maisha yao pasipo wenyewe kwenda spidi.

Nina ushauri mmoja kwa akina dada kwa sababu wao ndiyo waathirika wakubwa wa umbeya. Hii ni kwa sababu akinababa kidogo wana nafuu. Wanasikiliza na kushiriki umbeya, lakini hawajali, yaani kwao mambo yanaishia hapohapo kijiweni, wachache wanaoweka kichwani, ni wale ambao fainali imeshawakuta!
Shiriki umbeya, kwa sababu wakati mwingine hauwezi kuukwepa, lakini kuwa na akili ya ziada. Siyo kila utakaloambiwa ni baya, hapana.
Yapo mengine ni mazuri, yaweke na yafanyie kazi, lakini nina uhakika, kwa asilimia zaidi ya 80, wanawake wanaongea mambo yasiyowasaidia, yaani huyu ana vile, yule ana hivi, wale wanafanya hivi na mambo mengine kama hayo.
Usiwasikilize na kuwaamini. Jione kama uko peke yako na kila anayekuzunguka ni adui. Kuwa makini na unachokiongea mbele yao, na usiwe wakala wa kusambaza kinachozungumzwa nao. Ukiwa hivi, utajiweka salama.
Na hata ukiletewa umbeya, kwamba unasemwa vibaya na huyu, usiwe na haraka ya kuamua mambo, wakati mwingine kusemwa vibaya na kuyaacha kama yalivyo ni baraka.Ila nikusisitize kitu kimoja, mwanamke ana nafasi kubwa zaidi ya kufanikiwa kimaisha duniani kuliko mwanaume, kwa sababu amepewa kila kitu, hasa uwezo wake wa kumshawishi mwanaume amsaidie kufikia ndoto zake!

MIMI ‘MTU WANGU MZUNGU’ NDIYO NINI SASA? - 2

Karibuni sana wasomaji wangu wapendwa katika safu hii maalum kwa ajili ya kuelekezana mambo mbalimbali yanayohusu maisha kwa ujumla hasa upande wa mapenzi kama siyo mahaba.Mfano wa mambo hayo ni namna wenza wanaoishi na ndugu au wazazi wao wanavyopaswa kuishi kwa hekima bila kuwakwaza.
Kujiepusha na kauli zisizofaa ambazo mara nyingi zimekuwa zikiharibu uhusiano wao, kujiweka katika mazingira ya usafi wa nyumba na mavazi.Mambo mengine ni kuwa waaminifu katika uhusiano wao kwa sababu wenza wakiwa na michepuko huweza kuleta maradhi ndani ikiwa ni pamoja na migogoro inayosababisha kuachana.
KWA NINI UZUNGU UAMBATANE NA USALITI?
Wiki iliyopita tuliishia kwenye neno hili; ni sababu mbaya sana kusema ‘mtu wangu Mzungu’. Kisa hakuchunguzi, hakufuatilii.
Wengi wanaotoa madai au sifa hizo ni wale wasio na uadilifu na siku zote watu wasio na uadilifu ndiyo wanafurahia sana maisha ya kutofuatiliwa.Ukimwona mtu anasema mtu wake ni Mzungu maana yake ana mambo yake mengi ya siri lakini hayafuatiliwi kiasi cha kuwa kukamatwa au kujulikana nyendo zake.
Hii sifa imeshamiri sana katika jamii ya ‘Kiswahili’. Lakini wewe msomaji wangu ambaye upo katika uhusiano, chukulia kwamba, una mwenza anakusaliti lakini wewe hujui kwa sababu hufuatilii na unaitwa Mzungu. Je, siku ukijua Uzungu utauonaje?
 DHANA MBAYA KUWA NZURI
Mambo ya kutofuatiliwa yanaambatana na mawazo ya ubaya kuwa mzuri. Kwa nini nasema hivi? Kuna watu wanadiriki kusema hadharani maneno haya:“Mimi bwana simu yangu mwenzangu hashiki kabisa. Mimi sishiki yake na yeye hashiki yangu.”Hawa wanaosema hivi ni wana ndoa zaidi. Wanamwagiana sifa kwa kila mmoja kutoshika simu ya mwenzake, kwamba ni sifa kwao.
Lakini kusema ule ukweli, hata wewe msomaji tafakari kwa makini sana ukitumia akili za ndani. Je, ni sawa kwa wanandoa kuogopana kwenye simu? Mna nini cha siri ambacho mwenzako hatakiwi kushika?
 
MZUNGU MWENYEWE SASA
Kama utamkuta Mzungu anayesifiwa kwa kutokuwa na tabia ya kufuatilia mambo ya watu, atakwambia sababu kubwa ni kuamini.Niliwahi kuzungumza na mtu (Mzungu) mmoja anaitwa Frank, alisema kuwa, kwa Wazungu mtu kufumaniwa ni nadra sana kwani walio wengi ni waaminifu.
Alisema Wazungu wanaofumaniwa historia zao zinaonesha kuwa, alishatoka Uzunguni na kwenda kuishi mbali na kujikuta akibeba tabia za ugenini.Kwa hiyo ninapenda kumalizia mada yangu leo kwa kusema kwamba, matumizi  ya neno ‘mi mtu wangu Mzungu’ yasiambatane na usaliti wowote. Wapo wenza ambao hawaaminiki si kwa sababu wasiowaamini wana tabia za wivu uliopitiliza, bali kwa sababu ya matukio mbalimbali ya usaliti ya hao wasioaminika!
KUNA HULKA YA USALITI
Mbaya zaidi ni pale baadhi ya wenza kuwa na hulka ya usaliti. Wapo ambao hata akinaswa akisaliti si dawa ya kuachana na tabia hiyo, hao ndiyo wale ambao hupenda kuwaita wenza wao Wazungu. Tujisahihishe kuhusu hilo.Huu mwisho wa makala hii, tuungane wiki ijayo katika makala nyingine.


KIPINDI CHA ME & YOU WITH LOVE: AMANDA-NAPENDA MWANAUME ANIBUSU SHINGONI (PART- I)

 

Mtangazaji wa Kipindi cha Me & You Love, Shorvieny Mohamed (kushoto) kupitia Global TV Online akiwa katika pozi na mwigizaji mwenye figa ya aina yake Bongo Movie, Tamrina Posh 'Amanda' kabla ya kuanza mahojiano.
 
 Tamrina Posh 'Amanda' akiwa katika pozi wakati wa mahojiano.
KIPINDI kipya kutoka Global TV Online cha Me & You Love with Love kwa mara ya kwanza kimeanza kuonekana hewani kuanzia leo Alhamisi Februari 12, 2015. Kipindi hiki kinachotangazwa na Shorvieny Mohamed kitakuwa kikiwaunganisha mastaa, watu mashuhuri, wanasiasa na wengine wengi kuongelea uhusiano wa kimapenzi.
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI

JOTI wa Orijino Komedi Amwisha Pete Ya Uchumba Mpenzi Wake Wa Siku Nyingi!

Kwa mujibuwa mtandao wa  JF, Mwigizaji  wa vichekesho Lucas Mhuvile, almaarufu kama Joti, anayepiga kazi kwenye kampuni ya Orijino Komedi, amemvisha pete mpenzi wake wa ......

siku nyingi, ikiwa ni ishara na dalili njema kwamba safari ya kuelekea kwenye taasisi muhimu zaidi duniani ya NDOA imewadia..

Akiwa na swahiba wake wa siku nyingi, Mr. Mjuni Sylvatory a.k.a Mpoki, Joti alionekana mwenye furaha muda wote kwa kutimiza tendo hilo huku akiwa amealika watu wachache sana kuhudhuria tukio hilo.

Bongomovies.com bado haijazithibitisha taarifa hizi.

Kama ni kweli, tunampongeza sana na kumtakia kila la kheri yeye pamoja na mwenza wake
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI

Mambo Muhimu 11 Unayopaswa Kumwambia Mpenzi Wako Kila Siku.

Kutengeneza uhusiano wenye nguvu ni moja ya mambo yenye changamoto kubwa. Japo hakuna maelekezo maalum, kuna mambo machache na rahisi ambayo unaweza kumwambia mpenzi wako yakaujenga zaidi. Weka desturi ya kusema mambo haya kwa mpenzi wako na muda mfupi tu mtakuwa couple itakayowapa wivu marafiki zetu.
1. Nakupenda
teenagers-in-love-full-hd-wallpaper-metro-subway-love-you-kiss-1080p
Nakupenda ni kitu rahisi na cha wazi cha kumwambia mpenzi wako. Hakikisha tu kuwa unamaanisha. Jaribu kulisema neno hilo pindi mpenzi wako anapokuchekesha au pale anapofanya kitu kinachokukumbusha kwanini mko pamoja.
2.Nilikuwa nakuwaza
10599147_903366153015634_662713905701071893_n
Ni muhimu kumjulisha mpenzi wako kuwa unamuwaza hata kama hamko sehemu moja. Ukiona kitu kizuri au cha kuchekesha katika siku yako ambacho kinakufanya umkumbuke, mjulishe.
3. Siku yako ilikuaje?
day
Muulize masuala ambayo mpenzi wako anakutana nayo katika shughuli za kila siku. Muulize kuhusu huyo mfanyakazi mwenzie anayemkera au kazi kubwa waliyokuwa wakifanya. Kumpa nafasi mpenzi wako kushare sehemu zingine za maisha yake kutasaidia kuunganisha dots kati ya muda mnaokuwa pamoja.
4. Nakuunga mkono
hands-344759_640Mpe moyo mpenzi wako kwa kumjulisha kuwa unaunga mkono maamuzi yake. Unaweza ukaenda mbali zaidi kwa kujaribu kumsaidia afanikishe malengo aliyojiwekea. Maisha yamejaa vikwazo vingi, na ile hisia kuwa una mtu mwingine upande wako zinaweza kukusaidia kuvivuka. Msiwe couple tu, kuweni timu. Kumkumbusha mpenzi wako kuwa upo nyuma yake kutaimarisha uhusiano wenu.
5.Umependeza
Picha na OGS Studio
Kama umekuwa kwenye uhusiano kwa muda mrefu, ni rahisi kujisahau katika mengi. Ni muhimu kumkumbusha mpenzi wako kuwa anakuvutia. Kumjulisha kuwa ‘gauni hilo limekupendeza sana’ kutamfanya ajisikie vizuri na kukumbusha kwanini ulimchagua yeye.
6. Samahani
sorry
Kila mtu hukosea wakati fulani. Wakati mwingine hujikuta tukiongea maneno kwa hasira na baadaye kugundua kuwa hatukuwa sahihi. Ubishi hauna nafasi kwenye uhusiano wenye furaha, hivyo omba msamaha unapofanya kosa. Omba msamaha kwa kukasirika. Omba msamaha kwa kuumiza hisia za mpenzi wako. Omba msamaha hata kwa vitu ambavyo sio kosa lako.
7. Hakuna kama wewe
together-332260_640
Mpenzi wako anatakiwa kuwa rafiki yako. Kama hautaki kutembea naye, basi hamkupaswa kuwa kwenye uhusiano. Mfanye mpenzi wako ajue kuwa yeye ni bora na hakuna kama yeye.
8. Napenda mawazo yako
10487242_868433526508897_8354345900860777385_n
Picha: OGS Studio

Mwambie mpenzi wako kuwa unapenda mawazo yake. Mjulishe kuwa unaona ana akili, mcheshi, anajua kupenda na ana kipaji.
9.Nakuheshimu
couple-254683_640
Kama ulivyo uhusiano wa marafiki, heshima ni kitu muhimu kwako na mpenzi wako. Mpe nafasi ya kukushauri au kukupa mawazo kwenye mambo yanayokutatiza. Mtu anapohisi anaheshimiwa, hujisikia pia furaha na salama, vitu ambavyo ni muhimu kwenye uhusiano wowote mzuri.

10. Napingana na hilo
Sehemu moja wapo ya kumheshimu mpenzi wako ni kumjulisha pale usipokubaliana naye. Hakuna mtu anapenda kuoa mtu anayekubaliana na kila kitu na hakuna mwanamke anayetaka kuzaa watoto na mwanaume asiye na msimamo. Mnaweza kuwa timu, lakini nguvu ya timu yoyote ipo kwenye mawazo na matendo ya kila mmoja. Kuwa na maoni yako na yaseme kwa mtindo wa heshima. Kumpa mpenzi wako mtazamo tofauti kunaweza kumsaidia kupata suluhisho kwa tatizo ambalo hakuwa ameliwaza.
11. Usiku mwema
sleep-330869_640
Tunaishi kwenye wakati ambapo mawasiliano ni rahisi mno. Kwa kubonyeza tu kitufe tunaweza kutuma ujumbe kuvuka bahari, hivyo hakuna kisingizio cha kushindwa kusema ‘usiku’ mwema.
Haimjulishi mpenzi wako tu kuwa unataka kulala, bali pia inamjulisha kuwa unamfikiria. Hata kama hamjaongea siku nzima na hasa kama mmejibizana, maliza siku na kishindo chanya.
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI

KIPIGO KINAWEZA KUMNYOOSHA MWENZI WAKO?-2

Ni Jumatatu nyingine nzuri tunapokutana katika uwanja wetu huu, nakukaribisha kwa moyo mkunjufu ujumuike nami jamvini. Wiki iliyopita, tulianza kujadili mada yetu kama inavyojieleza kwa kuhoji kwamba kipigo kinaweza kusaidia kumnyoosha mwenzi wako?
Nianze kwa kukushukuru wewe ambaye ulituma ujumbe wako mfupi wa maandishi (SMS) ukichangia mada hii. Maoni yako ni ya muhimu sana na binafsi nimejifunza kitu kikubwa kutoka kwako.
WENGI WANACHUKIA SANA KUPIGWA
Wanawake wengi waliopo ndani ya ndoa na wale ambao bado hawajaingia kwenye ndoa, inaonesha kwamba hakuna kitu wanachokichukia kama kupigwa na wenzi wao.
Wapo ambao wametoa ushuhuda wa jinsi walivyoamua kukatisha ndoa zao kwa sababu ya vipigo na ubabe wa waume zao. Wengine wameeleza jinsi walivyoamua kuwakimbia wenzi wao bila taarifa, kwa sababu ya kuchoshwa na vipigo na manyanyaso ndani ya ndoa.
Nilichokibaini ni kwamba hakuna mtu anayependa kupigwa, kutukanwa au kunyanyaswa na mwenzi wake kwa sababu tu ya mapenzi. Kama wewe ni mwanaume na unataka kudumu kwenye ndoa yako, acha mara moja tabia ya kumpiga mwenzi wako.
KIPIGO HUONGEZA KIBURI
Kingine nilichokibaini, wanawake wengi hubadilika kitabia na kuwa wajeuri au wenye kiburi, kwa sababu ya kupigwa na wenzi wao.
“Kama nimefanya makosa, ni bora mume wangu anirekebishe kwa upole, mimi ni mtu mzima naelewa. Lakini akijifanya kutumia nguvu kwa kunipiga au kunitukana, kile alichonikataza nitakifanya maradufu,” huo ni ujumbe kutoka kwa msomaji wangu, Mama Zahoro wa Unguja, Zanzibar.
Kingine cha kujifunza hapa, kama wewe mwanaume kuna jambo hulipendi kuhusu mke wako, kama kweli unataka abadilike, usitumie ubabe au ukali kumrekebisha, zungumza naye kwa upole na bila shaka atakuelewa na kubadilika.
KWA WANAOJITAKIA KUPIGWA
Katika msafara wa mamba, kenge pia wapo. Wakati wanawake dunia nzima wakiunganisha nguvu kupinga ukatili dhidi yao, wapo wengine ambao kwa makusudi kabisa wanajitakia kupigwa na waume au wenzi wao.
Wengi inakuwa ni kwa sababu ya malezi waliyolelewa au maisha waliyowahi kupitia kabla ya kuwa na wenzi wao. Wanaume wengi waliotuma meseji kwangu, walionesha kwamba huwa hawapendi kuwapiga wenzi wao lakini wanalazimishwa kufanya hivyo kutokana na matendo ya wenzi wao.
UFANYEJE ILI USIPIGWE NA MUMEO?
Jibu ni jepesi sana, kitu cha kwanza; wanawake wanapaswa kujiepusha kujibizana na waume au wenzi wao inapotokea kuna ugomvi. Badala ya kuanza kupeana mipasho na mumeo utafikiri unasutana na shoga yako, ni vizuri kunyamaza hata kama unaonewa mpaka hasira zenu ziishe kisha ndiyo mjadiliane kwa upole.
Pia epuka kufanya jambo ambalo mwenzi wako ameshakukataza zaidi ya mara moja. Ukishajua mumeo hapendi ukae vibarazani kutwa ukipiga umbeya, ni vizuri kujitahidi kujizuia kwani ukishindwa kufanya hivyo, huenda ukaamsha hasira zake ukasababisha upigwe.
MWANAMKE HUPIGWA KWA UPANDE WA KHANGA
Mwisho ningependa kusisitiza nilichokieleza awali; tabia ya kupigana kwenye mapenzi siyo nzuri kwa watu wanaopendana ambao wana ndoto za kuishi pamoja kwa maisha yao yote. Kama ulikuwa na tabia hiyo, badilika, jifunze kukabiliana na hasira zako na badala ya kumtwanga mkeo kwa mangumi, muadhibu kwa kumfanyia kitu kizuri. Wahenga wanasema mwanamke hapigwi bali kwa upande wa khanga mpya.
Tukutane wiki ijayo kwa mada nyingine nzuri.
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI.

Mke afumaniwa, amgeuzia kibao mume wake Polisi



Jamaa mmoja alisababisha kizaazaa baada ya kuvamia chumbani ambako mtu na mkewe walikuwa wamelala.

DARASA LA MAHABA..!! KUNA UBAYA GANI KUFUATILIA NYENDO ZA MPENZI WAKO?

Ni wiki nyingine tulivu kabisa tunakutana kupitia safu hii nikiamini umzima na unaendelea nyema na maandalizi ya sikukuu za Christmas na Mwaka Mpya.

WANAOFICHA ‘MAKUCHA’ KABLA YA NDOA NI HATARI ZAIDI!

NIJumanne nyingine, namshukuru Mungu ameniwezesha kuifikia kwa namna yoyote ile!
Jumanne yetu ya leo tutakuwa na mada isemayo ‘wanaoficha ‘makucha’ kabla ya ndoa ni hatari zaidi’.

DARASA LA MAPENZI:ANGALIA MBINU MPYA ZA WANAWAKE WA SIKU HIZI WANAO SAKA NDOA KWA NGUVU...NI NOMA SANA

Siku ya kwanza atakuja na chupi 2, moja anaifua anaacha bafuni,nyingine anavaa asubuhi
anaondoka...

Umesikia hii ya Busu la Dada wa bwana harusi kuvunja ndoa siku ya harusi? Imetokea

busu
Hili nalo limeonekana kuchukua uzito mkubwa baada ya ndoa kuvunjika kanisani wakati mdogo wa kike wa bwana harusi alipoamua kwenda mbele na kumkiss kaka yake mbele ya bibi harusi kama ishara ya kuwapongeza.

WENGI WANAPENDA HARUSI KULIKO NDOA

NI Jumanne nyingine njema na inayompendeza Mwenyezi Mungu katika uumbaji wake. Mimi niko mzima wa afya njema ndiyo maana namwagika tena kwenye safu hii. Mada yetu wiki iliyopita ilisema; Mwanamke wa kumuoa hana sifa ya kuwa mke. Wengi walinipigia simu wakipongeza, wengine wakinikandia kwamba si kweli. Akisha kuwa mpenzi anaweza kuwa mke na akaendelea kuwa mpenzi.

MRISHO NGASSA NA LADHIA WAMEREMETA JIJINI DAR


Mrisho Ngassa na mkewe Ladhia Mngazija wakiwa na nyuso za tabasamu baada ya kufunga ndoa leo.  
MSHAMBULIAJI wa Taifa Stars na Yanga SC, Mrisho Ngassa leo amefunga ndoa ya pili na Ladhia Mngazija eneo la Tegeta jijini Dar es Salaam.

FAIDA, HASARA ZA WAPENZI KUFANYA KAZI OFISI MOJA -2

 


Mada iliyopo mezani ni faida na hasara za wapendao kufanya kazi ofisi moja ambayo tulianza kuijadili wiki iliyopita. Uhali gani msomaji wangu? Ni matumaini yangu kwamba unaendelea vizuri na majukumu ya ujenzi wa taifa. Karibu tena kwenye busati letu ambapo tunajuzana mambo mbalimbali yahusuyo mapennzi.

PICHA ZA UCH*I ZA KAHABA AKILIWA TIGO NA MUME WA MTU

MISS, MUMEWE WAZICHAPA

MREMBO Mariam Mohamed ambaye alishiriki na kushika nafasi ya pili ya Shindano la Miss Mara mwaka 2003, wiki iliyopita alizusha vurumai kubwa kwa kuzichapa kavukavu na mumewe usiku baada ya kumkuta akiwa na baamed ndani ya nyumba moja iliyopo Njiro eneo linalojulikana kama Nguzo Moja jijini Arusha, Amani lina mkanda kamili. 

KAMAUNAMPENDA MVUMILIE, KAMA KUACHA UTAACHA WANGAPI

 
Mpenzi msomaji wangu, huko mtaani kuna watu ambao wamekuwa wakipachikwa majina mabaya kutokana na tabia zao. Wapo ambao wanaitwa malaya kwa sababu kila mara wamekuwa wakibadili wapenzi.

CHUMBANI ZAIDI: MAMBO YANAYOCHANGIA KUPOTEZA HISIA ZA MAPENZI!

UKWELI ni kuwa watu wengi wanaodai hawatosheki katika mapenzi,ni wale wanaoziachia akili zao zitake tendo la ndoa zaidi.Watu hao hawaangalii uwezo,nafasi,hisia na afya ya kukutana kimwili.

MAPENZI NOOMA YAANI BINTI WA KIHINDI ANAPIGWA MZIGO NA KIJANA MWEUSI LIVE

Kumekuwa na msisimko mkubwa katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii nchini Kenya kuhusu taarifa ya msichana wa Kihindi aliyekiuka mila na tamaduni za jamii yake na kuolewa na kijana Mwafrika.

HIZI NDIO SABABU ZINAZOWAFANYA WANAWAKE WENGI WATAMANI KUOLEWA NA MWANAUME MPOLE.

Ukimuuliza binti yeyote mwenye ndoto ya kuolewa,akutajie sifa za mume ampendae,sifa ya "awe mpole" itakuwa ktk orodha ya mwanzo kabisa. Katika utafiti binafsi sifa hii imetajwa na wasichana 74 ikiwa ya kwanza,,wasichana 113 ikiwa ya 2.
© Copyright BONGO HABARI
Back To Top