Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

MECHI ZA LEO KATIKA LIGI KUU YA ENGLAND

 
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI

IVORY COAST YATINGA FAINALI AFCON 2015

 
Kipa wa DRC, Kidiaba akijaribu kuokoa mpira wa kichwa ulipigwa na Gervinho bila mafanikio. Hata hivyo mpira huo uliokolewa na mchezaji wa DRC ukielekea nyavuni.
KIKOSI cha Ivory Coast kikiongozwa na nahodha wake, Yaya Toure kimefanikiwa kutinga katika fainali za michuano ya Afcon 2015 baada ya kuichapa DR Congo mabao 3-1 katika mechi ya nusu fainali iliyopigwa usiku huu Equitorial Guinea.
Wafungaji wa mabao ya Ivory Coast walikuwa Yaya 21', Gervinho 41', Kanon 68' huku bao la DR Congo likifungwa na Mbokani 24' kwa penalti.
Kwa matokeo ya usiku huu, Ivory Coast wanasubiri mshindi wa mechi ya kesho kati ya Ghana na Equitorial Guinea kucheza naye katika fainali itakayopigwa Februari 8, mwaka huu.
DR Congo wanasubiri atakayefungwa kwenye mechi ya kesho ili wacheze naye Februari 7, mwaka huu kwenye mchezo wa kuwania nafasi ya tatu na ya nne.
 USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI

ARSENAL YAICHAPA 'MKONO' ASTON VILLA

 
Mesut Ozil akiifungia Arsenal bao la pili dakika ya 56.
 
Theo Walcott  akishangilia baada ya kuifungia Arsenal bao la tatu dakika ya 63.
 
Santi Cazorla akifunga bao la nne kwa mkwaju wa penalti katika dakika ya 75.
ARSENAL imeibuka na ushindi mnono wa mabao 5-0 dhidi ya Aston Villa leo kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya England uliopigwa Uwanja wa Emirates jijini London.
Mabao ya Arsenal yamewekwa kimiani na Olivier Giroud dakika ya 8, Mesut Ozil dakika ya 56, Theo Walcott dakika ya 63, Santi Cazorla dakika ya 75 na Hector Bellerin aliyefunga la mwisho muda wa nyongeza.
VIKOSI:
Arsenal: Ospina, Bellerin, Mertesacker, Koscielny, Monreal, Coquelin, Ramsey, Walcott, Cazorla, Ozil, Giroud
Benchi: Szczesny, Gibbs, Gabriel, Rosicky, Flamini, Chambers, Akpom
Aston Villa: Guzan, Hutton, Okore, Clark, Richardson, Delph,Gil, Sanchez, Cleverley, Benteke, Weimann
Benchi: Sinclair, Baker, Bacuna, Agbonlahor, Westwood, Cissokho, Given
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI 

Real Madrid yaomba CD tano za Isihaka, Messi wa Simba

SIMBA haina mwenendo mzuri katika Ligi Kuu Bara lakini kuna neema kidogo kwa wachezaji wake; beki wa kati Hassan Isihaka na straika Ramadhan Singano aliyewahi kupachikwa jina la Messi.
Neema yenyewe imekuja baada ya klabu ya Real Madrid ya Hispania kuomba CD tano za picha zao za video wakiichezea Simba katika mechi za hivi karibuni.


Maofisa wa Real Madrid ambao wapo nchini, wameuomba uongozi wa Simba uwapatie CD hizo za wachezaji hao ili watazamwe vizuri kabla ya kuwapa nafasi ya kufanya majaribio katika timu yao ya vijana.


Bosi mmoja wa Simba aliliambia Mwanaspoti akisema: “Real Madrid wametuomba hizo CD za Isihaka na Messi ili wazione na wakiridhika zaidi watawachukua kwa majaribio katika timu zao za vijana.”


Maofisa hao wa Madrid ambao wapo nchini kuanzisha mradi wa kituo cha kukuza soka la vijana, waliona uwezo wa Isihaka na Messi katika mchezo wao dhidi ya Azam FC wikiendi iliyopita ambao ulimalizika kwa sare ya bao 1-1.

Endapo jambo hilo litakuwa na mafanikio itakuwa neema kwao na kwa klabu
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI 

MALI, IVORY COAST NAZO ZATINGA ROBO FAINALI AFCON

 
Mali wakipambana na Guinea.
TIMU za Mali na Ivory Coast nazo zimefanikiwa kutinga hatua ya Robo Fainali ya Kombe la Mataifa Afrika 2015 kutoka Kundi D huku Guinea na Cameroon wakiyaaga mashindano hayo.
Ivory Coast wakipongezana kwa ushindi dhidi ya Cameroon usiku huu.
Mali wamesonga mbele baada ya sare ya bao 1-1 dhidi ya Guinea huku Ivory Coast wakiwachapa Cameroon bao 1-0.
Kwa matokeo hayo Mali na Ivory Coast zimeungana na Ghana, Algeria, Congo, Equitorial Guinea, Tunisia na DR Congo katika hatua ya robo fainali.
Katika hatua hiyo ya robo fainali, DR Congo watavaana na Congo, Tunisia na Equitorial Guinea, Ghana na Mali huku Algeria wakikipiga na Ivory Coast.
 USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI

SIMBA YACHAPWA NA MBEYA CITY TAIFA

Simba SC wakimenyana na Mbeya City katika Uwanja wa Taifa jijini Dar. (Picha na Maktaba Yetu)
SIMBA SC imeendelea kupoteza michezo yake hasa ya nyumbani baada ya leo kukubali tena kichapo cha mabao 2-1 dhidi ya Mbeya City.
Mechi hiyo ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) imepigwa muda mfupi uliopita katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Simba hivi karibuni ilipoteza mechi yake ya nyumbani baada ya kupigwa na Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Taifa, Dar kabla ya kutoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Azam FC majuzi.
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI

Daktari: Moyo wa Okwi ulisimama

Mshambuliaji Emmanuel Okwi akibebwa baada ya kuzimia.
MOYO wa mshambuliaji Emmanuel Okwi ulisimama kwa sekunde kadhaa alipogongwa kisogoni na beki Aggrey Morris wa Azam FC.
Okwi aligongwa katika mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Azam FC iliyomalizika kwa sare ya bao 1-1 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, jana.Daktari wa Simba, Yassin Gembe, amesema moyo wa Okwi ulisimama kwa sekunde kadhaa kutokana na pigo la kisogoni karibu kabisa na ubongo katika eneo la Medullar Oblangata.
“Hakikuwa kitu kidogo, tulilazimika kufanya tiba ili kurudisha mapigo ya moyo wake kwa kuwa ulisimama kwa sekunde kadhaa. Aliumia na uliona akitoa mapovu. “Baada ya hapo, tuliona ni vema kumfikisha Muhimbili ambako vipimo vyote vimefanyika. Imeonekana hakuumia sana na ameruhusiwa.
“Lakini mimi nimeamua kumpumzisha kwa siku mbili ili kuangalia kama atakuwa katika hali gani maana mwanzo unaweza kuona yuko vizuri kumbe kuna tatizo. “Ikionekana anaendelea vizuri, basi ataanza mazoezi lakini atakuwa chini ya uangalizi wangu,” alisema Dk Gembe.
Mshambuliaji wa Simba, Dan Sserunkuma alitumia muda mwingi kumlaumu Morris kwamba alishiriki kumpiga Okwi kiwiko, hata hivyo, alikuwa akikanusha.Okwi alibebwa haraka na kutolewa uwanjani na baadaye kukimbizwa Muhimbili ikiwa ni baada ya kuzinduka.
Kugongwa huko kwa Okwi, jana jioni kulizua gumzo kwa mashabiki wa soka nchi hasa wa Simba ambao walikuwa wakipiga simu katika ofisi za gazeti hili wakidai mabeki wamekuwa wakatili kwa washambuliaji.
 Wengi walitolea mfano wa beki George Michael wa Ruvu Shooting kumkaba mshambuliaji Amissi Tambwe wa Yanga.
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI

PIQUE, SHAKIRA WAFANYA BONGE LA PATI, MASTAA WAKIONGOZWA NA MESSI WAHUDHURIA

Beki Gerard Pique na mzazi mwenzake Shakira wamefanya bonge la pati kusherekea miaka miwili ya mtoto wao Milan.
Wachezaji kibao wa Barcelona, wakiongozwa na Lionel Messi, Luis Suarez na wapenzi wao walihudhuria pati hiyo iliyokuwa na ulinzi mkali.
 
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI

AZAM FC, SIMBA SC NGUVU SAWA TAIFA

TIMU ya Simba SC na Azam FC zimeshindwa kutambiana leo katika mechi ya Ligi Kuu Bara baada ya kutoka sare ya bao 1-1.
Katika mechi hiyo iliyopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar, bao la Simba limefungwa na Emmanuel Okwi dakika ya 19 wakati la kusawazisha la Azam likifungwa na Kipre Tchetche dakika ya 57.
Mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi alitolewa uwanjani kwenye machela baada ya kujeruhiwa na kukimbizwa hospitali.
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI

KIKOSI CHA AZAM KITAKACHOKWAANA NA SIMBA LEO

 
1. MWADINI ALI
2. SHOMARI KAPOMBE
3. ERASTO NYONI
4. AGGREY MORIS
5. PASCAL WAWA
6. BOLOU MICHAEL
7. MUDATHIR YAHYA
8. FRANK DOMAYO
9. DIDIER KAVUMBAGU
10. KIPRE TCHETCHE
11. HIMIDI MAO

BENCHI
1. KHALID MAHADHI
2. SAID MORAD
3. GADIEL MICHAEL
4. KELVIN FRIDAY
5. KHAMISI MCHA
6. AMRI KIEMBA
7. JOHN BOCCO

USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI

YANGA YAINOA POLISI MORO 1-0 UWANJA WA JAMHURI MKOANI MOROGORO

Mshambuliaji wa Yanga, Danny Mrwanda akipongezwa na mwenzake Kpah Sherman baada ya kuifungia timu yake bao pekee dhidi ya Polisi Moro jana.
Danny Mrwanda (kati) akijaribu kumtoka mchezaji wa timu ya Polisi Moro jana.
Kikosi cha timu ya Yanga.Kikosi cha timu ya Polisi.Mchezaji wa Polisi Moro akimtoka mchezaji wa timu ya Yanga.
TIMU ya Yanga SC jana ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Polisi Morogoro katika mechi iliyopigwa Uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro. Bao pekee la Yanga liliwekwa kimiani na mshambuliaji Danny Mrwanda.
(PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS / GPL, MOROGORO)
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI

Robin Van Persie na mtoto wake wa kiume walivyocheza soka kwenye tangazo la TV

Van Persie
24F925E800000578-0-image-a-17_1422010266198 
Mshambuliaji wa Manchester united Robin Van Persie ameshare freestyle ya  video akiwa na mtoto wake wa kiume Shaqueel mwenye umri wa miaka 7 wakiwa wanafanya mazoezi ya kutengeneza tangazo jipya la video kwa ajili ya kampeni ya BT Sport.
Star huyo wa Netherlands ameonekana katika video tatu tofauti  akimfundisha mtoto wake  baadhi ya mbinu za mpira kwenye kampeni hii iitwayo The father and son ambapo Robin ni balozi wa kampuni hiyo.
24F8F63900000578-0-image-a-19_1422010406117
24F923D800000578-0-image-a-20_1422010413826
24F925E800000578-0-image-a-17_1422010266198
24F9241600000578-0-image-a-16_1422010217351

USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI

RATIBA YA FA CUP LEO 24/01/2015 IKO HAPA...

 
 
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI

Exclusivee...SAMATTA AANZA MAZOEZI ULAYA ...AFUNGA GOLI MBILI...TAZAMA HAPA AKIWA MAZOEZINI



15922_870694186307442_880608052995095050_nHatimaye nyota ya mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania anayekipiga katika klabu ya TP Mazembe Mbwana Samatta imeanza kung’ara katika anga ya kimataifa ya soka.
Taarifa zilizothibitishwa ni kwamba mshambuliaji huyo yupo kwenye majaribio katika klabu ya CSKA Moscow – moja ya klabu kubwa kabisa nchini Urusi ambayo kwa miaka kadhaa imekuwa ikitawala soka la nchi hiyo na kucheza katika michuano ya mabingwa wa ulaya.

10690055_930864356931841_364362052221467735_n
Samatta alipewa nafasi ya kufanya majaribio ya siku 3 na klabu hiyo kwenye kambi yao ya mazoezi iliyopo Spain, lakini sasa ameongezewa wiki moja ya ziada ili maofisa wa jopo la ufundi la timu hiyo wapate muda wa kumuangalia vizuri.
Katika moja ya mechi za majaribio alizoichezea CSKA – Mbwana tayari amefunga magoli mawili.
10689498_930864360265174_71847191900962169_n
Pamoja na CSKA Moscow – timu nyingine ambazo zinatajwa kumtaka mshambuliaji huyo ni Inter Milan na Udinese za Italia, Atletico Madrid ya Spain, FC Basel ya Uswis na Kaiserslauten ya Ujerumani.
 CSKA Moscow
Mbwana 3
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI

Hii ya Romario wa Brazil na mpenzi wake mpya nayo imo leo…. miaka 19?

Romario 
Mshambuliaji nyota wa zamani wa Brazil Romario ametoa kali ya mwaka baada ya kuanza uhusiano nab inti mdogo mwenye umri kama wa kumzaa mwenyewe.
Romario anadhaniwa kuwa alianza uhusiano na mrembo mwenye umri wa miaka 19 Dixxie Pratt ambaye ni raia wa Marekani siku hache baada ya kuachana na mkewe mwaka 2014 .
Romario mwenye umri wa miaka 48 akiwa na mpenzi wake mpya mwenye umri wa miaka 19.
Romario mwenye umri wa miaka 48 akiwa na mpenzi wake mpya mwenye umri wa miaka 19.
Romario mwenye umri wa miaka 48 amemzidi Dixie kwa miaka 30 na binti huyo wala hakuwa amezaliwa wakati Romario akiiongoza Brazil kutwaa ubingwa wa dunia mwaka 1994 ambapo alikuwa moja kati ya wafungaji bora .
Romario atakumbukwa sana kwa mabao yake akiwa na timu ya taifa ya Brazil pamoja na klabu kadhaa ikiwemo Barcelona ambayo aliichezea baada ya kutwaa kombe la dunia mwaka 1994 .
Romario na mpenzi wake aitwaye Dixie wakiwa mazoezini kwenye ufukwe wa bahari huko Brazil.
Romario na mpenzi wake aitwaye Dixie wakiwa mazoezini kwenye ufukwe wa bahari huko Brazil.
Hivi karibuni kurasa mbalimbali binafsi za Mitandao ya kijamii za Romario zimekuwa zikirusha picha mbalimbali zikiwaonyesha Romario na Dixie wakiwa kwenye furaha ndani ya uhusiano wao .
Hapa wakiwa 'viwanja' kwenye 'bata'.
Hapa wakiwa ‘viwanja’ kwenye ‘bata’.
romario 4
Wakati Romario akiisaidia Brazil kutwaa ubingwa mwaka 1994 , mpenzi wake wa sasa Dixie alikuwa hajazaliwa.
Wakati Romario akiisaidia Brazil kutwaa ubingwa mwaka 1994 , mpenzi
wake wa sasa Dixie alikuwa hajazaliwa.
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI

Ishu ya Ronaldo na mpenzi wake, mwisho wa yote ni huu hapa…

Cristiano-Ronaldo-and-Irina-Shayk 
Kwa muda wa kama wiki mbili kumekuwa na story juu ya kuvunjika kwa uhusiano ya mwanasoka bora wa dunia, Cristiano Ronaldo na mpenzi wake ambaye ni mwanamitindo, Irina Shayk.
Wiki iliyopita msemaji rasmi wa Irina Shayk alithibitisha kwamba mrembo huyo mwenye asili ya Urusi ameachana na Ronaldo ambaye alikuwa na uhusiano naye kwa muda wa miaka 5, hata hivyo tetesi juu ya chanzo cha kuvunjika kwa uhusiano huyo zikaendelea huku mama mzazi wa Cristiano Ronaldo akitajwa kuhusika.
Mama mzazi wa Ronaldo, Dolares ametajwa kumkataa Irina kwa sababu haoni kama mwanamke huyo atafaa kuwa mzazi mwema kwa mtoto wa Ronaldo aitwaye Cristiano JR.
Cristiano I
Hata hivyo baada ya kusubiri kwa muda mrefu hatimaye Cristiano Ronaldo ameibuka na kuthibitisha kwamba ameachana na Irina huku akiomba jamii imuache aendelee na maisha yake binafsi.
Katika taarifa aliyotoa leo kwa vyombo vya habari, Ronaldo alisema ; “Huu ni mwisho wa uhusiano wangu na  Irina Shayk baada ya kudumu kwa miaka mitano. Tunaamini uamuzi huu ni sahihi kwa wakati huu
Cristiano II
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI

AZAM TV Kutokuonyesha Fainali za AFCON Mnaboa, Hatuitaji Uchambuzi Bila Kuona Mpira

Labda ni mimi tu ila kinachoendelea Azam Tv Kwenye Hizi fainali za AFCON kinaboa sana , yaani ile Chanel ya Azam 2 ambayo tulitegemea ituletee uhondo huo wa mpira haifanyi hivyo badala yake imeweka wachambuzi ambao wanaongea tu dakika tisini bila kuonyesha mpira wenyewe unaochezwa, kibaya zaidi kuna Kituo kimoja katika package ya Azam tv inayoitwa UBC siku mbili hizi Tatu zilikuwa zinaonyesha fainali hizo , leo ukiweka hiyo channel ya UBC inasema Channel Restricted ikiwa na maana wameizuia ili tusione mpira kwa maana tuendelee kuwaangalia tu wachambuzi wao wa Azam 2 bila kuona mpira....

Hivi kituo kikubwa cha michezo kama nyie kweli mmekosa leseni ya kuonyesha huo mpira??
Haingii akilini
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI

ARSENAL FC YATEMBELEA PSPF KWA LENGO LA KUSAKA FURSA ZA MAHUSIANO YA KIBIASHARA

Mkurugenzi Mkuu wa PSPF Bw. Adam Mayingu akimkabidhi zawadi  Mkurugenzi wa  Mahusiano ya kimaendeleo wa Klabu ya Arsenal Bw. Sam Stone (Kulia) , kushoto ni  Bw. Daniel Willey, Meneja wa Mahusiano ya Kimaendeleo ya Arsenal.  
Mkurgenzu Mkuu wa PSPF Bw. Adam Mayingu (kushoto) akimkabidhi zawadi Afisa Mtendaji Mkuu wa EAG Group, Bw Imani Kajura ambaye ni mwenyeji wa maafisa kutoka klabu ya Arsenal ambao wapo nchini kwa ajili ya kukutana na wadau mbalimbali kwa lengo kufungua mahusiano ya kibiashara.
Mkurugenzi wa Mahusiano ya kimaendeleo wa Klabu ya Arsenal Bw. Sam Stone (Kulia) akimkabidhi jezi ya timu hiyo Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF Bw. Adam Mayingu. Kushoto ni Bw. Daniel Willey, Meneja wa Mahusiano ya Kimaendeleo ya Arsenal. Maafisa hao wapo nchini kwa lengo la kukutana na wadau mbalimbali ili kufungua mahusiano ya kibiashara, katika mpango huo makocha wa timu hiyo na baadhi ya nyota waliowahi kuchezea timu hiyo watapata fursa kutembelea Tanzania. Klabu ya Arsenal ni kati ya klabu maarufu ulimwenguni ambayo inashiriki ligi maarufu duniani ya Barclyas
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI
© Copyright BONGO HABARI
Back To Top