Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

CHAZ BABA: SAJENT AMEGOMEA MWANANGU

PREZIDAA wa Bendi ya Mashujaa Musica, Charles Gabriel ‘Chaz Baba’ amefunguka kuwa anatamani kuishi na mwanaye aliyezaa na mwigizaji Husna Idd ‘Sajent’ lakini mzazi mwenziye huyo amekuwa akimgomea.

 
Prezidaa wa Bendi ya Mashujaa Musica, Charles Gabriel ‘Chaz Baba’ akiwa kwenye ofisi za Global Publishers.
Akizungumza na paparazi wetu, Chaz Baba alisema kabla hajaoa alikuwa akimg’ang’ania akae naye lakini alipooa, amegeuka na kukataa katakata.
“Kiukweli simuelewi kabisa Sajent maana katika hali na akili ya kawaida tu, sijaona mantiki ya kumkatalia mtoto wangu labda angeniambia kama mwanangu amekataa mwenyewe hapo kidogo nisingekuwa na swali,” alisema Chaz Baba.
 
Mwigizaji wa tasnia ya filamu Bongo, Husna Idd ‘Sajent’ aliyezaa na Chaz.
Chaz Baba ambaye alikuwa akibanjuka na Sajent miaka ya nyuma, kwa sasa ni mume halali wa ndoa na bi dada anayefahamika kwa jina la Rehema.

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright BONGO HABARI
Back To Top