BAADA
ya tetesi kuzagaa mitaani kwamba wasanii wa filamu Bongo, Wastara Juma
na Bondi Bin Salim wanatoka kimapenzi, bidada huyo ameibuka na kufunguka
kuwa bado hajamkubalia jumla Bondi kwani bado anamchunguza.
Wasanii wa filamu Bongo, Wastara Juma na Bondi Bin Salim.
Akipiga stori na paparazi wetu, Wastara alisema anamrekebisha baadhi
ya vitu ili aweze kuwa wake na kama hatabadilika, atampiga chini.
“Bondi ninamchunguza kwanza na kumpiga msasa awe wa tofauti na
alivyokuwa zamani sijamtangaza rasmi kwa sababu kuna vitu bado
sijajiridhisha kwake na naendelea kuvifanyia kazi nikijiridhisha basi
ndani ya mwaka huu nitamtangaza rasmi,” alisema Wastara.
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI
Get Free Email Updates to your Inbox!
Post a Comment