Katika mchezo wa raundi ya tatu ya kombe la FA dhidi ya timu ya Yeovil Town kocha Louis Van Gaal aliwashuhudia mabeki wa pembeni Rafael Da Silva na Luke Shaw wakitoka nje huku wakiwa na majeraha yanayohofiwa kuwa ya muda mrefu .
Beki Rafael amevunjika mfupa wa taya .
Beki mwingine wa kushoto Luke Shaw aliumia kifundo cha mguu wake baada ya kuwa anacheza kwa maumivu kwa muda mrefu na baada ya kushindwa kuvumilia alilazimika kutoka uwanjani.
Beki wa kushoto Luke Shaw ameumia ‘enka’.
United bado inaendelea kuwakosa wachezaji kadhaa wa kikosi cha kwanza kutokana na majeruhi akiwemo kiungo Mholanzi Daley Blind na beki Muargentina Marcos Rojo.
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI.
Post a Comment