NABII wa Kanisa la The Revelation lililopo Buza Kipera jijini Dar, Yaspi Bendera amesema uchaguzi mkuu ujao utakuwa balaa kubwa kufuatia maono anayoyaona wakati akishiriki ibada katika nyakati mbalimbali, Risasi Jumatano linakupa mkanda kamili.
“Nilimuona katika maono yangu kama mtu aliye kwenye majaribu makubwa kiroho, nikaandaa maombi hapa kanisani na tukamuombea kwa muda wa nusu saa na tunashukuru Mungu hali yake inaendelea vizuri baada ya kufanyiwa upasuaji wa tezi dume nchini Marekani. Bado namuona akiwa na maumivu kuanzia sehemu za kiuno, uti wa mgongo na shingoni mwake.
Waandishi wetu waliokuwa eneo la tukio walimshuhudia Nabii Yaspi akiwa ameshika picha ya Rais na waumini wake wakizama katika maombi kwa ajili ya Rais Kikwete huku na walipomaliza alisema tatizo lake limemalizika.
Nje ya ukumbi wa kanisa, Nabii huyo alizungumza na waandishi wetu ambao walimuuliza kuhusu jinsi anavyoona kuelekea uchaguzi mkuu wa mwakani.Vipi kuhusu utafiti wa Twaweza
“Utafiti umefanywa vizuri na nadhani kila kitu kipo kama kilivyoainishwa, lakini kama walivyosema wenyewe kwenye ripoti yao, upepo unaweza kubadilika wakati wowote maana miujiza ya Mungu huja bila kutarajiwa,” alisema.Nani atashinda Urais?
Utafiti uliotolewa na taasisi hiyo ya Twaweza uliotolewa hivi karibuni, ulisema kuwa endapo Uchaguzi mkuu wan chi ungefanyika hivi sasa, Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa angeibuka mshindi, huku akifuatiwa kwa karibu na Waziri Mkuu wa sasa, Mizengo Pinda na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Wilbroad Slaa akiibuka katika nafasi ya tatu.
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI.
Post a Comment