Miss Tanzania 2013, Happiness Watimanywa akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani).
Mwenyekiti wa kamati ya Miss Tanzania, Hashimu Lundenga, akiwa kwenye hafla hiyo.
Happiness Watimanywa na Lundenga wakiwa meza kuu.
KISURA aliyeibuka kidedea kwa kushinda taji la Miss
Tanzania mwaka 2013, Happiness Watimanywa (20), kesho anatarajia
kuondoka nchini kuelekea Uingereza katika kushiriki mashindano ya
urembo ya dunia, yatakayofanyika jijini London kuanzia Desemba 14 mwaka
huu.
Hayo yamesemwa leo na Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania, Hashimu
Lundenga, alipokuwa akizungumza na wanahabari katika jijini Dar es
Salaam.Akizungumzia suala hilo, Happiness amesema:
“Nitajitahidi sana kuonekana katika hao warembo 130 watakaoshiriki
kwani nimejianda vizuri. Wadau na sekta mbalimbali zimeniandaa vya
kutosha wakiwemo wanamitindo wa hapa nchini kunivisha katika mashindano
hayo.”
(GPL)
Get Free Email Updates to your Inbox!
Post a Comment