Featured

    Featured Posts

    Udaku

    Social Icons

    Udaku

Loading...

DEREVA WA BODABODA NUSURA AMUUE MREMBO

DEREVA wa bodaboda aliyefahamika kwa jina moja la Fikiri, nusura amuue mrembo mmoja mkazi wa Tandale-Kwatumbo, jijini Dar baada ya kumparamia na bodaboda kando ya barabara.

 
Mrembo (jina halikufahamika mara moja) aliyenusurika kifo baada ya kugongwa na mwendesha bodaboda aliyefahamika kwa jina moja la Fikiri.
Katika tukio hilo lililotokea hivi karibuni, dereva huyo wa bodaboda akiwa anatokea upande wa Kwamtogole kuelekea Magomeni-Makanya, alipokaribia kona ya kuelekea Magomeni-Kagera ndipo akamvaa mwanamke huyo aliyekuwa akijipitia zake na kumfanya apoteze fahamu kwa dakika kadhaa.
 
Raia wakishuhudia ajali iliyotokea.
Chanzo kimeeleza kuwa, mwendesha bodaboda huyo alikuwa kasi ‘akamu-overtake’ mwenzake lakini baada ya kuchomoza mbele yake alikutana na bodaboda nyingine ambayo alivaana nayo na kwenda kumkumba mrembo huyo, akaanguka na kuzimia.
Bodaboda huyo na abiria wake mwenye asili ya kiarabu walitumbukia kwenye mtaro na kugalagala kwa dakika kadhaa kabla ya kuchomolewa na wasamaria wema.
 
Bodaboda ikiwa mtaroni baada ya ajali.
Baadaye mrembo huyo alizinduka na kusema kuwa mwendesha bodaboda huyo alimfanyia kitu mbaya sana kwa kuwa yeye alikuwa kando kabisa ya barabara lakini alishangaa bodoboda hiyo kumfuata alipo.

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright 2025 BONGO HABARI | Designed By Code Nirvana
Back To Top