Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

TAMASHA LA SAUTI ZA BUSARA KUFANYIKA FEBRUARI 12-15 ZANZIBAR

Mwenyekiti wa Bodi ya Tamasha la Sauti za Busara Simai Mohamed Saidi (wa pili kushoto) akizungumza.
Sehemu ya waandishi wa habari waliokuwa kwenye hafla hiyo.
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Ally Kiba (kulia) akielezea  namna alivyojipanga kuburudisha kwenye tamasha hilo.
…Akipeana  mkono na viongozi kwenye mkutano huo.
TAMASHA la Sauti za Busara  linatarajiwa kufanyika Februari 12 hadi 15 mwaka huu  huko Mji Mkongwe (Stone Town) Zanzibar.
Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, muandaaji wa tamasha hilo,  Dave Ojay Haashim,  alisema madhumuni  ya tamasha hilo ni kuwaweka pamoja watu kutoka sehemu mbalimbali  duniani ili kusherehekea muziki wa Afrika chini ya anga la Zanzibar ambapo pia kutakuwa na wasanii wa muziki wa kizazi kipya.
Tamasha hilo la 12 tangu kuanzishwa kwake limekuwa likifanyika kila mwaka kwa kuhusisha wasanii kutoka pande mbalimbali za dunia ambao huimba moja kwa moja jukwaani (live) kwa kutumia zana za muziki.
Naye Mkurugenzi wa Busara Promotion, Yusuf Mahmoud, alisema msimu huu jumla ya wasanii na vikundi 680 viliomba kushiriki lakini baada ya mchujo vilibaki vikundi 37 pekee.
Alisema kati yake 19 ni kutoka Tanzania na wengine wanatoka nchi mbalimbali wakiwemo Blitz The Ambassador mwenye asili ya Ghana anayeishi na kufanya kazi zake huko Brooklyn, Marekani.
Pia aliongeza kuwa  kutakuwa na filamu maalum kwa ajili ya kumuenzi Fatuma binti Baraka (Bi Kidude ) na kila mshiriki atatakiwa kuimba wimbo wa kuhamasisha amani na watatu watakaoimba vizuri watapewa tuzo pamoja na kitita cha Sh. milioni tisa.
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright BONGO HABARI
Back To Top