SIMBA haina mwenendo mzuri katika Ligi Kuu Bara lakini kuna neema kidogo
kwa wachezaji wake; beki wa kati Hassan Isihaka na straika Ramadhan
Singano aliyewahi kupachikwa jina la Messi.
Maofisa wa Real Madrid ambao wapo nchini, wameuomba uongozi wa Simba uwapatie CD hizo za wachezaji hao ili watazamwe vizuri kabla ya kuwapa nafasi ya kufanya majaribio katika timu yao ya vijana.
Bosi mmoja wa Simba aliliambia Mwanaspoti akisema: “Real Madrid wametuomba hizo CD za Isihaka na Messi ili wazione na wakiridhika zaidi watawachukua kwa majaribio katika timu zao za vijana.”
Maofisa hao wa Madrid ambao wapo nchini kuanzisha mradi wa kituo cha kukuza soka la vijana, waliona uwezo wa Isihaka na Messi katika mchezo wao dhidi ya Azam FC wikiendi iliyopita ambao ulimalizika kwa sare ya bao 1-1.
Endapo jambo hilo litakuwa na mafanikio itakuwa neema kwao na kwa klabu
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI
Post a Comment