Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

HAFSA AELEZA ALIVYO-TESWA NA MAUZAUZA


MWANAMUZIKI aliyeamua kumgeukia Mungu na kuokoka, Hafsa Kazinja amefunguka kuwa alikuwa akiteswa na mauzauza ya kishirikina pindi alipokuwa katika majukwaa akiimba Bongo Fleva.
Mwanamuziki aliyeamua kumgeukia Mungu na kuokoka, Hafsa Kazinja.
Akipiga stori na paparazi wetu, Hafsa alisema alikumbana na mambo mengi sana ya ajabu ikiwemo kuona majoka makubwa jukwaani akiwa anatumbuiza na sauti za ajabu za mara kwa mara. 
Hafsa Kazinja akipozi.
“Nilikuwa naishi maisha ya ajabu sana jamani yaani, nikiwa jukwaani naimba basi naanza kusikia sauti za ajabu mara naona majoka makubwa yanapita pita mbele yangu na kunifanya niishiwe pozi katika utumbuizaji wangu, hayo yote najua zilikuwa chuki za binadamu, nashukuru tangu niokoke hivi sasa sina matatizo hayo kabisa,” alisema Hafsa.
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright BONGO HABARI
Back To Top