Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Mufindi, Paulo Ntinika (mwenye bluu) alipokuwa akisikiliza tuhuma dhidia yake
Akajaribu kujitetea lakini hakueleweka
Mwenyekiti wa Halmashauri ya
Wilaya ya Mufindi, Peter Tweve (aliyekunja ngumi) akisistiza makosa ya
baadhi ya watumishi wa halmashauri hiyo
Mweka Hazina wa halmashauri hiyo, Athumani Kihamiya ambaye sasa ameteuliwa kukaimu nafasi ya ukurugenzi
Fedha hizo, kwa mujibu wa taarifa
iliyotolewa kwa wanahabari na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Peter
Tweve zinahusu kazi za ujenzi zilizoongezwa na watendaji wa halmashauri
hiyo kinyume na maelekezo ya sheria ya manunuzi namba 40(1) ya mwaka
2005.
Katika kikao hicho kilichofanyika
juzi, baada ya madiwani wa halmashauri hiyo (wote wa CCM) kujadili suala
hilo katika kikao cha chama chao siku moja kabla, baadhi yao walisikika
wakitoa kauli zinazomkataa mkurugenzi huyo.
Na wengine (bila kutaja majina
yao) waliomba vyombo vya dola vimchukulie hatua za kisheria kwa madai
kwamba za kinidhamu pekee hazitoshi kutoa onyo kwa wengine.
Kabla ya kikao hicho hakijafikia
maamuzi dhidi ya wahusika wote waliosababisha hasara ya fedha hizo, hali
ya kiafya ya Ntinika ilidaiwa kubadilika ghafla jambo lililosababisha
akimbizwe katika hospitali ya wilaya hiyo kwa ajili ya matibabu.
Baada ya kupewa ushauri na
matibabu, Ntinika ambaye ni kama amepumzishwa kwa muda usiojulikana
kuendelea na majukumu yake hayo ili kupisha kilichoelezwa na Mwenyekiti
wa halmashauri hiyo "uchunguzi utakaoainisha wahusika wote wa ubadhilifu
wa fedha hizo" hakurudi tena katika kikao hicho kilichomteua mweka
hazina wa halmashauri hiyo, Athumani Kihamiya kukaimu nafasi ya
ukurugenzi.
Wakati hayo yote yakitokea
wanahabari waliohudhuria kikao hicho, walitolewa nje baada ya baraza
hilo la kawaida kugeuzwa na kuwa kamati maalumu ya baraza hilo
iliyojadili taarifa ya kamati ya ukaguzi ya wilaya kwa siri.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo ya
ukaguzi ya Julai Septemba 2014/2015 ambayo nakala yake tunayo, baadhi ya
barabara zinazohusishwa na malipo ya nyongeza ni pamoja na ya Kibengu
hadi Kipanga yenye urefu wa km 37, barabara ya Kipanga B hadi Uhafiwa na
barabara ya Mkuta Ludilo hadi Ilasa yenye km 21.
Kwa mfano, barabara ya Kibengu
Kipanga, taarifa hiyo ya ukaguzi inaonesha Januari 1, 2014 kikao cha
zabuni kilikaa na kutoa kazi ya nyongeza yenye thamani ya Sh 21,876,500
kwa ajili ya matengezo yake na kufanya thamani ya kazi yote kuwa Sh
313,956,500.
Hata hivyo taarifa hiyo inaeleza badala ya Sh 21,876,500 iliyopitishwa na bodi ya zabuni, kazi hiyo iliongezwa Sh 85,029,500.
"Kama halmashauri tumeazimia
wahusika wote waliofanya matumizi nje ya utaratibu wachukuliwe hatua za
kinidhamu. Wakati hayo yakiendelea tunaomba wananchi wawe na subira
kuona ni taratibu zipi zitafuatwa," alisema.
Alisema kamati ya fedha ndiyo
itakayofanya kazi ya kuainisha watumishi wanaohusika na tuhuma hiyo na
kwamba taarifa yake ya kile kitakachopatikana itatolewa Novemba 24.
Tweve alisema halmashauri hiyo
itatoa taarifa kwa mamlaka zingine zinazohusika ili wahusika
watakaobainika kuhusika wachukuliwe hatua nyingine za kisheria.
Alisema sula la mkurugenzi wa
halmashauri hiyo kuendelea au kutoendelea na nafasi yake hiyo litaamliwa
na mamlaka za juu ambazo tayari zimejulishwa kuhusu kile kinachoendelea
wilayani humo.
"Jambo muhimu ni kwamba, katika
kujiridhisha na tuhuma hizi, tumebaini kuna mambo hayakufuatwa kwa
mujibu wa taratibu na sheria. Kwahiyo kama mkurugenzi , mhandisi au
mhasibu na yoyote yule ambaye ni mtumishi wa halmashauriikithibitika
amehusika watachukuliwa hatua za kinidhamu," alisema.
Akizungumzia utaratibu wa sheria
ya manunuzi Tweve alisema wakandarasi huingia mikataba na halmashauri
baada ya kushinda zabuni zilizotangazwa.
"Kwa mujibu wa sheria
wanakandarasi wanatakiwa kufanya kazi zilizopo kwenye mkataba na kwa
malipo yaliyopangwa na kama kuna kazi ya nyongeza mkuu wa idara
anatakiwa apeleke maombi kitengo cha manunuzi kitakachoitisha kikao cha
bodi ya manunuzi ili kilidhie nyongeza ya kazi," alisema
Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri
hiyo, aliwataka wananchi wawe wavumilivu akiwaahidi ufumbuzi wa suala
hilo kujulikana katika kipindi kilichowekwa.
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI.
Post a Comment