Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

Migomo yaendelea kutikisa kila kona nchini Tanzania ambapo Tabora wafanya biashara nao wagoma.

Wananchi manispaa ya Tabora wamekuwa katika wakati mgumu wa kununua bidhaa mbali mbali baada ya wafanyabiashara  wa maduka yote ya maeneo ya soko kuu mjini humo,  kufanya mgomo wa kushitukiza wakiishinikiza serikali kwa mambo matatu, ya kumpa dhamana mwenyekiti wao kitaifa,Bw.Johnson Minja,kuongezeka kwa kodi asilimia mia moja,na matumizi ya mashine za EFDS.
Wakiongea na ITV katika  sehemu za maduka hayo akiwemo Mwenyekiti wa wafanyabiashara hao wamesema kuwa, hali ambayo imewafanya kugoma ni kutokana na malalamiko yao kutosikilizwa kwa mda mrefu, pamoja na juhudi ambazo zimekuwa zikifanywa na viongozi wao jambo ambalo limekuwa ni kitendawili huku wakiongezewa kodi. 
 
Akizungumza na wafanyabiashara hao mwenyekiti wa kamati ya ukusanyaji wa kodi wilaya hiyo ya Tabora mjini, ambaye pia ni mkuu wa wilaya hiyo Bw.Suleimani Kumchaya,amewataka kutokuwa na maamuzi yanayoathiri jamii bali kufanya makubaliano yanayoleta maendeleo katika jamii,kuliko kuchukua hatua za maamuzi na za haraka.

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright BONGO HABARI
Back To Top