Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

Matusi na ngumi zatawala baraza la wawakilishi Zanzibar.

Wajumbe wa baraza la wawakilishi wameweka tofauti za seriklai ya kitaifa pembeni na kuanza kutupiana matusi na  kutishia kupigana hadharani ndani ya baraza baada ya mabishano kuhusu hoja ya vitambulisho vya Zanzibar.
Hali hiyo ambayo haijawahi kutokezea  ndani ya baraza hilo ilianza wakati wajumbe walipokuwa wakianza  kuchangia hoja hiyo binafsi ya mwakilshi wa CUF Mh. Hamad Masoud ambapo mwakishi wa CUF jimbo la magogoni Mh. Abdillahi Jihad ambaye pia ni waziri alipaonza kumshambulia wazir wa nchi tawala za mikoa na idara maalum  Mh. Haji Omar Kheir
 
Hapo ndipo sakata hilolilipoanza  ambapo  naibu  waziri amabye ni CCM Mh. Haji Gavu alipaona kukwaruzana kwamaneno na matusi dhidi ya mwakilishi wa CUF na kutaka kugeuza ukumbi huo kuwa wa masumbwi.
 
Pamoja na jitihada za spika Mh. Pandu Ameir Kificho kutaka kuwepo kwa amani na utaratibu hakiusaidii  lolote na fujo hizo zikageuka kwa wawakilishi wa CCM Mh. Hamza Hassan Juma na mwakilishi wa CUF Mh. Salum Nassor ambao mnao wataka kuzipiga na kutishiana kwenda nje.
 
Hili ni tukio la pili kutokea ndani ya mkutano huu wa baraza ambao wawakilishi wa CUF na CCM kuvutana na kubishana kwa maneno ya matusi na kejeli.

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright BONGO HABARI
Back To Top