Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

MIMI ‘MTU WANGU MZUNGU’ NDIYO NINI SASA? - 2

Karibuni sana wasomaji wangu wapendwa katika safu hii maalum kwa ajili ya kuelekezana mambo mbalimbali yanayohusu maisha kwa ujumla hasa upande wa mapenzi kama siyo mahaba.Mfano wa mambo hayo ni namna wenza wanaoishi na ndugu au wazazi wao wanavyopaswa kuishi kwa hekima bila kuwakwaza.
Kujiepusha na kauli zisizofaa ambazo mara nyingi zimekuwa zikiharibu uhusiano wao, kujiweka katika mazingira ya usafi wa nyumba na mavazi.Mambo mengine ni kuwa waaminifu katika uhusiano wao kwa sababu wenza wakiwa na michepuko huweza kuleta maradhi ndani ikiwa ni pamoja na migogoro inayosababisha kuachana.
KWA NINI UZUNGU UAMBATANE NA USALITI?
Wiki iliyopita tuliishia kwenye neno hili; ni sababu mbaya sana kusema ‘mtu wangu Mzungu’. Kisa hakuchunguzi, hakufuatilii.
Wengi wanaotoa madai au sifa hizo ni wale wasio na uadilifu na siku zote watu wasio na uadilifu ndiyo wanafurahia sana maisha ya kutofuatiliwa.Ukimwona mtu anasema mtu wake ni Mzungu maana yake ana mambo yake mengi ya siri lakini hayafuatiliwi kiasi cha kuwa kukamatwa au kujulikana nyendo zake.
Hii sifa imeshamiri sana katika jamii ya ‘Kiswahili’. Lakini wewe msomaji wangu ambaye upo katika uhusiano, chukulia kwamba, una mwenza anakusaliti lakini wewe hujui kwa sababu hufuatilii na unaitwa Mzungu. Je, siku ukijua Uzungu utauonaje?
 DHANA MBAYA KUWA NZURI
Mambo ya kutofuatiliwa yanaambatana na mawazo ya ubaya kuwa mzuri. Kwa nini nasema hivi? Kuna watu wanadiriki kusema hadharani maneno haya:“Mimi bwana simu yangu mwenzangu hashiki kabisa. Mimi sishiki yake na yeye hashiki yangu.”Hawa wanaosema hivi ni wana ndoa zaidi. Wanamwagiana sifa kwa kila mmoja kutoshika simu ya mwenzake, kwamba ni sifa kwao.
Lakini kusema ule ukweli, hata wewe msomaji tafakari kwa makini sana ukitumia akili za ndani. Je, ni sawa kwa wanandoa kuogopana kwenye simu? Mna nini cha siri ambacho mwenzako hatakiwi kushika?
 
MZUNGU MWENYEWE SASA
Kama utamkuta Mzungu anayesifiwa kwa kutokuwa na tabia ya kufuatilia mambo ya watu, atakwambia sababu kubwa ni kuamini.Niliwahi kuzungumza na mtu (Mzungu) mmoja anaitwa Frank, alisema kuwa, kwa Wazungu mtu kufumaniwa ni nadra sana kwani walio wengi ni waaminifu.
Alisema Wazungu wanaofumaniwa historia zao zinaonesha kuwa, alishatoka Uzunguni na kwenda kuishi mbali na kujikuta akibeba tabia za ugenini.Kwa hiyo ninapenda kumalizia mada yangu leo kwa kusema kwamba, matumizi  ya neno ‘mi mtu wangu Mzungu’ yasiambatane na usaliti wowote. Wapo wenza ambao hawaaminiki si kwa sababu wasiowaamini wana tabia za wivu uliopitiliza, bali kwa sababu ya matukio mbalimbali ya usaliti ya hao wasioaminika!
KUNA HULKA YA USALITI
Mbaya zaidi ni pale baadhi ya wenza kuwa na hulka ya usaliti. Wapo ambao hata akinaswa akisaliti si dawa ya kuachana na tabia hiyo, hao ndiyo wale ambao hupenda kuwaita wenza wao Wazungu. Tujisahihishe kuhusu hilo.Huu mwisho wa makala hii, tuungane wiki ijayo katika makala nyingine.


PAUL MAKONDA, DK SLAA WAMJULIA HALI ASKOFU GWAJIMA

 
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Wilibroad Silaa (kushoto), akimjulia hali Askofu Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda akimjulia hali Askofu Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima aliyelazwa Hospitali ya TMJ kwa ajili ya matibabu baada ya kupata mshituko katika mahojiano na polisi akituhumiwa kutoa lugha isiyofaa kwa Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo.
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Wilibroad Silaa (kushoto), akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda walipokutana Hospitali ya TMJ walipofika kumjulia hali Askofu Gwajima.

Baada ya Kuhamia Nyumba Mpya, Diamond na Zari Roho Mkononi, Yabainiki Kwake ulinzi ni Sifuri, Mwenyewe Akiri Kuishi kwa Hofu

TAHADHARI ichukuliwe! Habari zikufikie kuwa, baada ya staa mkubwa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz‘ na mpenzi wake, Zarinah Hassani ‘Zari’, kuhamia kwenye mjengo wake mpya uliopo Madale jijini Dar, imebainika kuwa familia hiyo inaishi roho mkononi kufuatia ulinzi sifuri, jambo linalowafanya kuishi kwa hofu tupu

Kikizungumza kwa hofu juu ya familia hiyo, chanzo chetu makini kilipasha kwamba, pamoja na Diamond kutumia mamilioni ya fedha kujenga nyumba hiyo ya gharama kubwa, sasa changamoto imehamia kwenye ulinzi na usalama wao

“Jamani watu wanampongeza Diamond kwa kuhamia nyumba mpya lakini wale jamaa aisee wanapaswa kuombewa kila kukicha.

“Pamoja na kushusha mjengo wa maana bado changamoto ni juu ya ulinzi wao.

“Huwezi kuamini Diamond bado anaishi kizamani sana na sijui kwa nini anajiamini kiasi hicho wakati anajua wazi kuwa yeye ni staa wa Afrika na hapaswi kuishi kwa ulinzi hafifu.

MAENEO HATARISHI?

“Nasema hivi kwa sababu hata maeneo anayoishi ni hatari sana kwake hivyo anatakiwa kuwa na ulinzi mkali ili tu siku moja asije akafanyiwa kitu ambacho taifa likaingia kwenye hasara ya kumpoteza nyota mkubwa kama yeye.

“Nina uhakika asilimia mia moja Diamond hadi leo hajaanza hata kufanya process (taratibu) za kuchukua silaha (bastola).

“Mimi naijua vizuri Madale ni sehemu ambayo watu huwa wanavamiwa mara kwa mara na wanaishi kwa hofu kama Diamond anavyoishi.

HIKI NDICHO KINACHOMPONZA

“Kitu kingine kinachomponza Diamond ni ishu ya kuweka kila kitu kilichopo ndani kwake mitandaoni. Usione kila mtu anasifia lakini kuna wengine wanavitolea macho.

“Kwa mfano katupia picha za toilet (choo) ambacho kimepakwa dhahabu na kusema kimegharimu shilingi milioni 70.

“Hajakaa sawa akatupia picha za jikoni kwake kuna vitu vingi vya thamani kubwa kila mahali mpaka kwenye korido kuna flat screen (runinga). Huko si ni kuwakejeli watoto wa mbwa? Ni vizuri akaacha kufanya hivyo kwa sababu anawapa watu tamaa,” kilitiririka chanzo hicho.

ANA ULINZI GANI?

Juu ya ulinzi wa nyumbani kwa Diamond, chanzo hicho kilidai kwamba, mbali na baunsa anayewalinda aitwaye Mwarabu hakuna askari wa silaha anayelinda nyumbani hapo hivyo jamaa anatakiwa kufanya haraka kuajiri walinzi wenye silaha.


Baada ya habari hizo na uchunguzi wa kutosha, Ijumaa Wikienda lilimsaka Diamond a.k.a Dangote au Chibu ili kujua namna anavyoishi na jinsi anavyoimarisha ulinzi wake na familia kwa jumla.

Diamond, mbali na kukiri kuwa na hofu, alikuwa na haya ya kusema: “Suala la ulinzi wangu nalijua mwenyewe lakini zaidi watu wanatakiwa kujua mimi nipo na mlinzi na ninaendelea kuimarisha ulinzi wa nyumbani kwangu.

“Sidhani pia kama ni suala zuri sana kwa watu kujua siri za ulinzi wangu ila mambo mengi ya kujilinda niko kwenye michakato ya mwisho kukamilisha na soon (haraka) mambo yote yatakaa levo maana huwezi ukafanya kila jambo kwa wakati mmoja,” alisema Diamond huku akikubaliana na ushauri wa gazeti hili juu ya kuongeza ulinzi alionao wa baunsa.

ILIWAHI KUMTOKEA SUGU

Huko nyuma iliwahi kumtokea Mwanamuziki Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ ambaye kwa sasa ni Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema) ambapo alikuwa amerejea kutoka nchini Uingereza.

Akiwa amepanga nyumba nzima maeneo ya Tegeta, Dar, Sugu alifanyiwa makala ya runingani na kuonesha vitu vya thamani vya nyumbani kwake.

Siku chache baada ya kipindi hicho kuruka runingani, jamaa huyo alivamiwa na kuporwa kila kitu lakini yeye hakudhurika.

Emmanuel Mbasha Afunguka sakata la Gwajima katika Twitter, Asema Hayuko Tayari Kurudiana na Mkewe

Katika Sakata linaloendelea sasa la Gwajima Kumtukana Askofu Pengo na la Kuzidiwa na Kukimbizwa Hospitalini akiwa mikononi mwa Polisi , Emmanuel Mbasha ambae inasemakana yeye na mkewe kuachana kuna mkono wa Gwajima ametoa maoni yake kuhusu Sakata la Askofu Huyo..
Jisomee Hapa Chini:

TAMKO LA MAASKOFU NA WACHUNGAJI KUTOKA MADHEHEBU MBALIMBALI JUU YA TUKIO LA ASKOFU GWAJIMA.

Sisi maaskofu na wachungaji kutoka makanisa mbalimbali tumeshtushwa na kusikitishwa kwa taarifa ya ugonjwa wa Askofu na mtumishi mwenzetu Josephat Gwajima ambaye tarehe 27/03/2015 alifika kituo cha polisi cha kati kuitikia wito wa polisi uliomtaka kwenda kujibu shutuma za kutumia lugha ya matusi kwa kardinali Pengo.
Maswali yetu makuu ni kitu gani kimempata mwenzetu? Tunajiuliza, je vyombo vya usalama vimekua sio sehemu salama kama zamani?
Tukiwa bado tunatafakari hill, tumeshtushwa tena baada ya kupata taarifa ya kuwa Wachungaji Wasaidizi wa Askofu Gwajima pamoja na walinzi wake waliokuwepo hospitalini hapo kwa ajili ya kumuuguza nao pia wamekamatwa kwa tuhuma za. kutaka kumtorosha Askofu Gwajima. 
Jambo hili linashangaza zaidi maana wachungaji wale wale waliokuwa naye akiwa mzima wa afya wakati anaelekea polisi ndio wale wale wanatuhumiwa kutaka kumtorosha akiwa mgonjwa.
Ni jambo la kushangaza na lisiloingia akilini kuwa wasaidizi hao wa Gwajima walitaka kumtorosha wakati Gwajima kama angekua na nia hiyo angekwisha fanya hivyo mana alikuwa na uwezo wa kutoroka alipokua Arusha kwenye kikao cha Maaskofu wakuu wa makanisa ya Kipentekoste ambao alipata taarifa za kuitwa Polisi.
Isitoshe Gwajima aliitija wito na kwenda polisi mwenyewe kwa miguu yake bila kushurutishwa, wala hakufikishwa polisi kwa nguvu.
Swali: Kama alikua anaona ugumu wa kutoroka wakati hakuna polisi anayemlinda na huku akiwa mwenye afya tele, itakuaje rahisi kutoroshwa leo akiwa mahututi na akiwa kwenye ulinzi mkali wa polisi?
Mbona hii inastaajabisha?
Jambo jingine linalotupa shida ni kuhusu mlalamikaji wa kesi hii inayomkabili Askofu Gwajima. Tumeelezwa na wasaidizi wa Askofu Gwajima kuwa pale polisi walielezwa kuwa aliyefungua kesi hii sio Pengo ila mtu mmoja aitwaye Aboubakar.
Kwa ufahamu wetu juu ya sheria unatutuma kuamini kuwa Aboubakar sio MTU sahihi wa kufungua kesi hiyo sababu hawezi kutuonyesha ameumizwa kiasi gani na matamshi ya Askofu Gwajima.
Isitoshe, Kardinali Pengo mwenyewe ametamka katika Ibada yake ya Jumapili hii ya tarehe 29/03/2015 kuwa amemsamehe Gwajima, yupi tena mwenye uchungu wa kumzidi Kardinali Pengo?
 RAI YETU:
Rai yetu ni kwamba, ni vizuri serikali pamoja na vyombo vyake vya usalama vikatumia weledi katika kushughulikia mambo ya kidini na viongozi wake kwani yanaweza kusababisha chuki dhidi ya serikali na pia kupelekea mpasuko mkubwa wa kidini katika jamii yetu iliyo na historia nzuri ya umoja na mshikamano na ushirikiano katika matukio yote ya kimaisha.
Tunaomba serikali isaidie kuondoa mkanganyiko huu na busara kubwa itumike ili kuepusha uvunjifu wa Amani katika jamii.
MAAMUZI YETU:
Jambo hili linazungumzika, maana hata hivyo tumeshaazimia kukutana na IGP ili kupata suluhisho juu ya jambo hili.
Kwa niaba ya maaskofu na wachungaji:
Mwenyekiti: Askofu Dr. Mgullu Kilimba
Katibu: Askofu Dr. Dramas Mukassa
Na mwandishi
F.A.K
30/03/2015

Gwajima Afunguka......Asema Aliagiza Bastola yake ili Ajihami Baada ya Taarifa Kuzagaa Mitandaoni kuwa Amefariki Dunia

Hii  ni  Picha  iliyosambazwa  katika  mitandao  ya  kijamii  ikidai  kuwa  Gwajima  kafariki  dunia  na  yuko  Mochwari.Taarifa  hizi  zilimpa  hofu  Gwajima  na  kumfanya  Aagize  Bastola  yake  kwa  ajili  ya  kujihami.
**********

Utata umeibuka kuhusu bastola waliyodaiwa kukamatwa nayo wafuasi wa Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Askofu Josephat Gwajima baada ya kiongozi huyo kusema anaimiliki kihalali kinyume na maelezo ya polisi.
  

Gwajima aliyetolewa kwenye chumba cha uangalizi maalumu cha Hospitali ya TMJ jana, amelitaka Jeshi la Polisi kurudisha bastola hiyo, akisema ni mali yake na aliiagiza ipelekwe hospitalini kwa sababu ya kujilinda.
 
Akizungumza na waandishi wa habari hospitalini hapo alipolazwa baada ya kuishiwa nguvu na kupoteza fahamu akiwa katika mahojiano na polisi, Gwajima alisema anashangaa kukamatwa kwa wachungaji wake waliokuwapo kwa ajili ya kumlinda.
 
Hata hivyo, katika kwa upande mwingine, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema bunduki hiyo haina umiliki halali wa Gwajima wala wa wachungaji 15 waliokamatwa lakini baadaye jioni baada ya maelezo ya Gwajima, alitoa taarifa akisema bastola hiyo ni mali halali ya askofu huyo. Pia alisema kuhusu risasi 17 za bunduki aina ya Shortgun, Gwajima anamiliki bunduki ya aina hiyo lakini akasema uchunguzi kuhusu watu hao 15 unaendelea.

Kauli ya Gwajima
Akizungumza kwa shida akiwa amejishika tumbo, Gwajima alisemaalipopata taarifa za uvumi kwenye mitandao ya kijamii kuwa amefariki dunia, aliagiza wachungaji waende hospitalini kwa ajili ya kumlinda, lakini wakaishia mikononi mwa polisi wakidaiwa kutaka kumtorosha.
 
Alisema alihofia kuwapo kwa watu wabaya ambao wangeweza kumdhuru halafu wakasingizia kitendo hicho kufanywa na polisi kwa kuwa alipata tatizo akiwa mikononi mwao.
 
“Usiku wasiwasi ulizidi, huku kila mmoja akiwa hafahamu kwa nini ujumbe wa namna ile unasambazwa kwenye mitandao, msambazaji ni nani, ana nia gani, nikaamua kuwaagiza waniletee silaha yangu iliyokuwa kwenye begi ili likitokea lolote niweze kujilinda,” alisema Gwajima.
 
Alisema alishangaa kukamatwa wachungaji wake na kuchukua silaha iliyokuwa ndani ya begi na hadi jana hakuwa ameulizwa chochote kuhusu umiliki wa silaha hiyo.
 
“Kabla sijazungumza na waandishi kueleza ukweli wa kinachodaiwa kuwa nilitaka kutoroshwa na wachungaji wangu, nilitaka kuzungumza na ZCO (Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalumu), lakini hajaja, kadi ya ile silaha ninayo,” alisema Gwajima.
 
Alisema madai kuwa alitaka kutoroka ilihali polisi alikwenda mwenyewe akitokea Arusha baada ya kusoma katika vyombo vya habari kuwa anatafutwa.
 
Alifafanua kuwa hata alipofika polisi kwa ajili ya mahojiano hakuwa na shaka hata kidogo, lakini alishangaa kuona anaishiwa nguvu kila baada ya muda na alipoona kichwa kinamuuma, akawaomba wampeleke hospitali ili mambo mengine yafuate baadaye, kitu ambacho hakikufanyika kwa wakati.
 
Wasiwasi kwa polisi
Alisema alijaribu kuomba apelekwe hospitali mara kadhaa, lakini hakuna aliyekubaliana naye hadi alipopoteza fahamu na kupelekwa hospitali ya Polisi Kurasini.
 
“Hivi hata kama ni chombo cha usalama, nimepata matatizo nipo mikononi mwao, halafu nikubali kutibiwa katika hospitali yao, sikulitaka hilo na hata waliposema nikatibiwe Muhimbili pia sikutaka, ndiyo maana nilikuja hapa, sisemi moja kwa moja kama Polisi wanahusika lakini kuna vitu vinanitia shaka,” alisema Gwajima.
 
Alieleza kuwa anatilia shaka Jeshi la Polisi kutokana na kuwapo vitu vingi vinavyoashiria wana kitu kingine wanatafuta, kwani jana tulikuwa na hofu ya kuvamiwa, waliokuja kutuvamia ni wao, sikugombana na Pengo, nilikuwa namkemea kama kiongozi mwenzangu wa kiroho wao, wameligeuza ni kesi.
 
“Sijawahi kulitilia shaka Jeshi la Polisi lakini katika hili napata wasiwasi mwingi, sina ugomvi na Kardinali Pengo, nampenda, hajanilaumu, wala kunishtaki, nilikuwa namkemea katika masuala yetu ya mabaraza ya dini na siyo vinginevyo,” alisema Gwajima.
 
Gwajima pia alionyesha wasiwasi wake kwa kile kilichokuwa kinang’ang’aniwa na polisi kwenda kupekua nyumbani kwake kuwa hakikuwa kitu kizuri.
 
Kova alipinga
Wakati Gwajima akisema hayo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema bastola waliyokutwa nayo wafuasi wa Gwajima haimilikiwi kihalali.
 
“Tumegundua kuwa katika wale watu waliokuwa pale akiwamo Gwajima mwenyewe, (bastola) haikuwa  katika umiliki wao halali, kwa hiyo hapa kuna kesi ya kupatikana na silaha bila kibali.”
 
Akizungumzia tuhuma kwamba polisi walimpekua mke wa Gwajima, Kova alisema hakuna polisi waliofika nyumbani kwake kufanya upekuzi wowote na kama wakitaka kufanya hivyo watafuata taratibu maalumu za upekuzi.
 
Akijibu swali kuhusu mahali Gwajima alipotakiwa kutoroshewa, Kova alisema uchunguzi huo bado unaendelea na utakapomalizika wahusika watafikishwa mahakamani.
 
Pia alipoulizwa kama Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo amemsamehe Gwajima, kwani polisi imng’ang’anie, Kova alisema;“amesema anamsamehe lakini haingilii mambo ya sheria.”
 
Kuhusu sababu za Gwajima kuzimia wakati akihojiwa, Kova alisema anayepaswa kuulizwa kwa nini alianguka wakati akihojiwa na polisi ni Gwajima mwenyewe.
 
“Siri za mahojiano huwa hazitolewi kabla ya ushahidi mahakamani, sababu ya kupata shock (mshtuko) atajua mwenyewe, kwa kuwa ukifanyiwa jambo ukafurahi au ukachukia wewe ndiyo unajua ilikuwaje, chochote kitakachotokea ukicheka, ukinuna, ukizimia, wewe ndiyo tukuulize ilikuwaje mpaka ukazimia kwa sababu hisia unazipata wewe,”alisema Kova.

Makonda amtembelea
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda ambaye alikuwa amemwandikia Gwajima barua akimwita ofisi kwake, jana mchana alimtembelea hospitalini hapo kwa ajili ya kumjulia hali kiongozi huyo lakini akasisitiza kuwa nia yake bado ipo palepale.
“Nilimtaka leo aripoti ofisini kwangu lakini kwa bahati mbaya anaugua na amelazwa. Nitakwenda kumuona ili nijue hali yake ikoje,” alisema Makonda kabla ya kufunga safari kwenda hospitali alikolazwa.
 
Alisema pia atataka kiongozi huyo wa kiroho amweleze anavyoelewa maana ya uhuru wa kuabudu unaoelezwa katika Katiba, usajili wa taasisi yake na katiba ya taasisi hiyo. 
  
“Mimi ni mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kinondoni. Niliagiza polisi wamkamate na baadaye wakimaliza kumhoji aje kwangu pia atahojiwa na jopo la watu 20,” alisema Makonda.

WATANO WANUSURIKA KIFO BAADA YA KUFUKIWA NA KIFUSI JIJINI MWANZA

Rashid Mkumba Hamis ambaye ni mmoja wa majeruhi aliyevunjika mguu.
Majeruhi katika tukio hilo wakihojiwa na wanahabari (hawapo pichani).
Vikosi vya uokoaji vikitoa msaada eneo la tukio.
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Baraka Kunisaga akiongea na wanahabari baada ya ajali hiyo.
Eneo la msingi uliokuwa unajengwa na kuangukiwa na ukuta.
Wananchi wakishuhudia tukio hilo.
Vijana wakijaribu kuokoa baadhi ya mali zilizofukiwa na kifusi hicho.

Watu watano katika Wilaya ya Nyamagana jijini hapa wamenusurika kifo baada ya kuangukiwa na kifusi wakati wakiwa kwenye maandalizi ya kujenga jengo lililotegemewa kuwa na ghorofa saba, eneo la Nyerere Road, leo majira ya saa sita mchana.
Akizungumza na waandishi wa habari eneo la tukio, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Baraka Kunisaga amesema kuwa amesikitishwa na tukio hilo ambapo watu hao wameangukiwa na ukuta wakati wakijenga msingi wa jengo hilo na hii ni kutokana na kuwa na wakandarasi ambao hawajengi majengo kwa kiwango kinachotakiwa.
Katika hatua nyingine, Kunisaga amesema kuwa hali ya Watanzania kuwa wanapoteza uhai wao kila kukicha kutokana na kuangukiwa na vifusi, serikali haiwezi kukubaliana nayo hivyo amesitisha ujenzi wa jengo hilo.
Majeruhi waliokumbwa na tukio hilo wameongea na waandishi wa habari japo kwa taabu na kusema kuwa ukuta uliowaangukia ulikuwa umeunganishwa kama uzio hivyo wakati wakiendelea kuchimba msingi, uzio huo ulikuwa ukiendelea kutitia hivyo kusababisha kuporomoka na kuwaangukia.
Daktari wa zamu wodi ya dharura, Ernest Elisenguo amethibitisha kupokea majeruhi watano ambao wametokana na tukio la kuporomokewa na kifusi na kuwataja kuwa ni Ramadhan Hussein Nyarandu, Rashid Mkumba Hamis, Elias Bahati, Benson Agustino na Mtani ambapo watatu kati ya hao hali yao imeendelea vizuri na wameruhusiwa kwenda nyumbani ila wawili kati yao bado hali zao siyo nzuri na wataendelea kuwa chini ya uangalizi wa madaktari.
Majeruhi Rashid Mkumba Hamis, ameeleza kama ifuatavyo: "Mimi ni fundi na  nilikuwa natengeneza 'bezi' kwa ajili ya kushikilia nguzo za ghorofa wakati ninaendelea na kazi yangu nikaanza kusikia udongo ukiniangukia mgongoni, ghafla nikasikia matofali yananiangukia.

Demi Lovato Shows Off Puppy, Bikini Body

 Demi Lovato Bikini Photo
Demi Lovato has unveiled a new Instagram photo that is both totally adorable AND drop dead sexy.
It features the 22-year old singer holding her puppy while flaunting her impressive bikini body, writing as a caption to the image... nothing. She just included a sun, palm tree and heart emoji.
Lovato, of course, spent many weeks in rehab a few years ago, partly over substance abuse issues and partly due to a battle with bulimia.
There was simply no way the old Demi Lovato would have posted a photo such as this.
But now?
"I love my butt," Lovato recently told Allure. "Hopefully it stays that way, because this thing isn't going anywhere."
About a month ago, meanwhile, Demi posted another swimsuit snapshot, writing along with it an empowering message to young women everywhere.
“Regardless of what society tells you these days… You don’t have to have a thigh gap to be beautiful," she penned, adding:
"It is possible to love your body the way it is. #fitness #health #acceptance #selflove."
Amen, sister.
Lovato also considers herself lucky for waking up alongside Wilmer Valderrama every morning.
Along with a cute photo of the couple, Lovato wrote on Instagram a few weeks ago:
"After sharing my ups, putting up with my downs and supporting my recovery... he still never takes credit and I want the world to know how incredible his soul is. I really wouldn't be alive today without him. I love you Wilmer."

TIWA SAVAGE, FLAVOUR, DAVIDO WASHINDWA KUPIGA KURA NIGERIA

Tiwa Savage.
WAKATI wananchi wa Nigeria wakiwa katika zoezi la kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika juzi na jana, baadhi ya mastaa walishindwa kuhudhuria tukio hilo muhimu kutokana na majukumu mbalimbali.
 
Davido Adeleke.
Miongoni mwa mastaa hao ni mwanamuziki Davido Adeleke, aliyekuwa na shoo kwenye tamasha moja nchini Kenya hivyo hakuweza kupiga kura.
Flavour N'abania.
Mwanamuziki mwingine Flavour N'abania yeye alikuwa jijini London kwenye Tamasha la Dance Afrique. Huku mastaa wengine wakiwemo Tiwa Savage na P Square wakihudhuria tamasha hilo.
 
Toke Makinwa.
Mtangazaji Toke Makinwa yeye alikuwa nchini China wakati wa tukio hilo.
Mwanamuziki Wizkid ni staa mwingine ambaye hakupiga kura kutokana na shoo yake aliyokuwa nayo huko Dubai.
Wizkid.
Matokeo ya uchaguzi huo yanatarajiwa kutangazwa leo jioni ambapo Rais Goodluck Jonathan wa chama tawala cha PDP na Muhammud Buhari kutoka chama cha upinzani cha APC wanachuana vikali.

WATANGAZA NIA WAELEWE KUWA RAIS WA AWAMU YA TANO ATABEBA MIZIGO MIZITO

Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
TUMSHUKURU Mungu kwa kutupa uhai, hatuna budi kumpongeza kwa kutupendelea kwani wengi kawachukua na sasa wametangulia mbele za haki.
Baada ya kusema hayo nianze mada ya leo kwa kusema kwamba  rais ajaye wa awamu ya tano hapa nchini atabeba mizigo mizito na kwa hali hiyo ni wazi kwamba atakuwa na wakati mgumu pengine kuliko watangulizi wake wanne.
Naamini kwamba wanasiasa wote waliotangaza nia ya kuwania ofisi hiyo kubwa kuliko zote nchini kiutendaji wanalitambua hilo, na wamejipima na kujiridhisha kuwa wako tayari kukabiliana na changamoto zinazotokana na jukumu hilo kubwa.
Mifano ni mingi ya jinsi atakavyokumbana na changamoto nyingi kama vile, itakuwa kazi ngumu kwake kuwafunga midomo Watanzania ambao kwa sasa wameelimika, wanajitambua pia wanafahamu haki zao, wanafahamu nini wanakitaka, nini wanakikosa na baadhi yao wanajua sheria za nchi.
Kiongozi ajaye, awe wa CCM au upinzani, hakuna shaka kazi yake ya kwanza itakuwa ni kuunda serikali,  jukumu ambalo pia siyo rahisi kama ilivyokuwa zamani pia atakuwa na jukumu la kutekeleza kazi zote zilizoanzishwa bila kukamilishwa na mtangulizi wake wa awamu ya nne, Rais Jakaya Kikwete.
Mbali ya ahadi za Kikwete, pia kuna masuala mengine mengi yamekuwa sugu na serikali yake imeshindwa kukabiliana nayo. Hayo ni pamoja na ujangili, rushwa, biashara ya dawa za kulevya, matumizi mabaya ya fedha za umma yaani ufisadi na mikataba mibovu inayoangamiza nchi.
Kuna matatizo mengi kama vile migogoro baina ya wakulima na wafugaji karibu maeneo mengi nchini na inasumbua wengi na kusababisha vifo katika baadhi ya sehemu kama yalivyoainishwa vizuri kwenye ripoti ya kamati teule ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyoongozwa na Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka.
Tatizo hili ni kubwa na zito linalohitaji ufumbuzi wa haraka. Ardhi, ni rasilimali kubwa, utajiri ambao nchi yetu imejaliwa kuwa nao, lakini imekuwa na mzozo hasa baada ya kuwaingiza wawekezaji ambao wanalalamikiwa na wananchi kutokana na kuingiza unyanyasaji.
Hapa nchini kwa sasa ardhi inauzwa hovyo wakati mwingine kwa kisingizio cha uwekezaji mkubwa au mdogo, dhuluma za kuwania viwanja au mashamba zinaongezeka, mijini na vijijini.
Ardhi, badala ya kuwa rasilimali, imegeuka chanzo, sababu kubwa ya ugomvi na maafa makubwa kwenye jamii zetu nyingi.
Matokeo ya maafa ya ardhi siyo madogo na haipo sababu ya kufumbiwa macho na kuachwa yapite, rais ajaye atakumbana na changamoto hii.
Mbali ya ardhi, kuna tatizo la mauaji ya Albino,wanawake kwa wanaume, hasa wenye umri mkubwa kutokana na ushirikina na  yamekuwa yakitokea Shinyanga, Mwanza au mikoa mingine ya kanda ya ziwa, hili ni tatizo ambalo rais ajaye lazima ahakikishe analimaliza.
Kuhusu watu wenye ulemavu wa ngozi (albino), ni wengi, wanaendelea kuwindwa kama vile wao ni swala wanaowindwa kwa ajili ya kitoweo, kisa ni dhana potofu kwamba ngozi zao ni biashara nzuri, yenye kuleta utajiri. Upuuzi huu ni kama mfupa mgumu ambao serikali ya awamu ya nne imejaribu kuutafuna, lakini imeshindwa, sasa utahamishiwa kwa rais ajaye.
Pia, kuna tatizo la Katiba Mpya ambayo inasubiriwa kupigiwa kura ya maoni siku si nyingi, lakini mchakato huo ukikwama litakuwa ni jukumu jingine la rais ajaye.
Nchi yetu, ambayo imejitangaza kama kisiwa cha amani, utulivu na mshikamano katika miaka ya karibuni imeshuhudia pia matukio mengi ya mauaji na uhalifu unaongezeka, ujambazi na udini umeanza kushamiri. Ni jukumu la rais ajaye kuona tatizo hili linalotishia amani ya nchi yetu nzuri.
Ukabila pia una harufu yake, hivi sasa kuna ukanda, hili ni tatizo zito ambalo rais ajaye atatakiwa atoe kucha kuliangamiza.
Jipu limepasuka, siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli.
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI

MFANYABIASHARA APIGWA...


MFANYABIASHARA wa Kisesa wilayani Magu, Mwanza, Nestory Andrew ameuawa kwa kupigwa risasi na majambazi usiku wa Februari 16, mwaka huu huku mke wake akishuhudia.
 
Mke wa mfanyabiashara huyo (kulia) akiwa na simanzi kubwa.
Imedaiwa kuwa kabla ya majambazi hao hawajafanya mauaji hayo, waliuteka Mtaa wa Kisesa kwani jirani na duka la mfanyabiashara huyo kulikuwa  na mafundi baiskeli ambao walizuiwa kupiga kelele na wauaji hao.
“Tukio hili lilitisha kwa sababu lilitokea mita kama 55 kutoka kituo cha polisi na hawakutoa msaada wowote,” alisema shuhuda mmoja.Akisumulia tukio hilo, mfanyakazi wa marehemu aitwaye Emmanuel Kulwa alisema bosi wake huyo alifika dukani saa mbili usiku ghafla wakati analifunga duka aliona mtu akiwa amevaa koti jeusi ambaye alipiga risasi kadhaa hewani, yeye akakimbia.
 
Nestory Andrew enzi za uhai wake.
“Baada ya hali kutulia nilirudi dukani nikakuta bosi wangu ameshauawa na mwili wake ukiwa umepelekwa Hospitali ya Mkoa  Sekeoture,” alisema.  Mke wa marehemu, Sara Limbu alisema alishuhudia tukio hilo la kuuawa mume wake baada ya kushuhudia risasi zikirindima eneo la tukio.
“Nilikimbia lakini nilirudi dukani baadaye na kumkuta mume wangu ameshafariki kwa kupigwa risasi mbili kifuani… ameniachia watoto sita. Mungu ailaze mahali pema peponi roho yake,” alisema mama huyo.
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI

MAITI YA MCHUNGAJI YAZUA TAFRANI

MAITI ya Mchungaji James Regnald Mhando  aliyefariki  Februari 18, mwaka huu imezua tafrani nzito kwa ndugu na jamaa baada ya kujulikana kuwa alikuwa na wake wawili ambapo mke mmoja alitaka mwili uagwe hospitali na upande wa pili ukitaka ukaagwe kwa mama yake marehemu.
 
Mchungaji James Regnald Mhando enzi za uhai wake.
Katika msiba huo ilibainika kuwa, mchungaji huyo (kanisa lake tunalihifadhi kwa sababu maalum), alikuwa na watoto sita kwa mama tofauti na wote walijitokeza katika mazishi ya baba yao.
Inadaiwa  kuwa Mchungaji Mhando alianza kuumwa Jumamosi ya Februari 14, mwaka huu lakini inadaiwa baadhi ya watoto na ndugu wengine hawakujulishwa hadi Jumanne ambapo inadaiwa alibebwa na gari la wagonjwa kutokea Morogoro hadi Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Jeneza la mchungaji James Regnald Mhando.
Habari zinasema ilipofika Jumatano saa tano usiku, mchungaji huyo aliaga dunia na mbali ya kuaga dunia, bado tukio hilo lilikuwa ni siri na ilidaiwa ilikuwa afanyiwe shughuli za mazishi kwa siri bila ya baadhi ya watoto wake wakubwa kujua.
Hata hivyo, habari za msiba huo zilizagaa haraka na kumfikia mke wa kwanza wa ndoa ambaye alikuwa nchini kwa ajili ya mapumziko kwani anafanya kazi nje ya nchi, hivyo ukoo ukaanza kutaarifiana.
Mchungaji Mhando alioa na kufunga ndoa Novemba 17,  1979  katika Kanisa la Anglikana la Mtakatifu Albano, jijini Dar es Salaam,  hata hivyo,  ilidaiwa kuwa mwaka 1985 mtumishi huyo wa Mungu aliamua kuondoka nyumbani alikokuwa akiishi na mkewe na kwenda kuishi na mwanamke mwingine ambaye inadaiwa kuwa alikuwa ni wa dhehebu lingine na wakafunga ndoa serikalini.
Habari zinadai kwamba mwanamke huyo alikuwa anaitwa Mwanaheri kabla ya kubadili dini na kuitwa Glory na wakafanikiwa kuzaa  watoto wawili, mmoja akapewa jina la Reginald Junior na mtoto mwingine anaitwa Sada au Doreen Mhando. Habari zinasema kabla ya kuondoka kwa mke wa kwanza, mchungaji huyo alizaa naye watoto wawili, wa kiume na wa kike....Askari akiwa eneo la tukio.
Hata hivyo, wakati wa msiba huo watoto wengine wawili walijitokeza nao wakidai kuwa ni baba yao, hali iliyozusha minong’ono kwa watu walioshangazwa na mwenendo wa marehemu.Akizungumza na Uwazi, mama mzazi wa mchungaji huyo aliyejitambulisha kwa jina la Dorofea Mhando (82) alisema kitendo kilichofanywa na mwanamke huyo ni kibaya kwani alimshawishi mwanaye kuisaliti familia yake.
“Mwanamke huyo mwingine alikuwa akiishi na mwanangu kwa siri kubwa  sana, kama vile marehemu hakuwa na familia na akawa anajifanya kuwa yeye ndiye mke wa kwanza, kitu ambacho ni cha uongo kwani marehemu alishaoa kanisani mwaka 1979.
“Marehemu baada ya kumpata mwanamke huyo alikuwa hashiriki shughuli nyingi za hapa nyumbani kwa kuhofia watu  watajua kuwa alikuwa na familia nyingine,  kitu ambacho kilinisikitisha,” alidai mama huyo.
Mwili wa marehemu ukiagwa.
Mama  huyo aliongeza  kuwa  maisha ya mchungaji huyo yalikuwa sehemu mbili, Morogoro na jijini Dar  es Salaam, alikuwa akifikia Mivinjeni kwenye ofisi ya shughuli zake.“Baada ya kupata taarifa ya msiba niliagiza mwili uletwe hapa Ukonga Majumba Sita ukitokea Muhimbili kwa ajili ya shughuli za kuagwa lakini mke mdogo akawa anapinga,” alidai mama huyo.
Hata hivyo, ilidaiwa kuwa mke mdogo alisisitiza kuwa baada ya kuandaa mwili wa marehemu uagwe Muhimbili, kisha  upelekwe katika Makabauri ya Kinondoni kwa mazishi.   Kulitokea mabishano ambapo mtoto mkubwa wa marehemu aliyefahamika kwa  jina Feda, alisema  baba yao hawezi  kuagwa kama mkimbizi kwani ana watoto, mke na mama yake mzazi, hivyo akaamuru mwili ukaagwe kwa bibi yake Ukonga Majumba Sita.
Habari zinadai kuwa mvutano huo ulifikishwa Polisi Kituo Kikuu ambapo lilifunguliwa jalada namba CD/ RB/ 2627/ 2015 ambao waliamuru shughuli za mazishi zisifanyike hadi muafaka upatikane.
Habari zinadai kikao kilifanyika polisi na muafaka ukapatikana kwamba mwili ukaagwe kwa mama yake mzazi Ukonga Majumba Sita.
Maofisa wa polisi walitoa askari wenye silaha chini ya kamanda wao aliyefahamika kwa jina moja la Manyama aliyeongozana na wana familia hao hadi Muhimbili kisha Ukonga, baadaye kwenye Makaburi ya Kinondoni ambapo mchungaji huyo alizikwa chini ya ulinzi.
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI

SHOGA: CHAKULA CHA USIKU KISILIWE GIZANI!

 
Asalaam alaykhum shoga yangu! Kama ilivyoada, leo ni Jumanne nyingine ambayo Mwenyezi Mungu amependa tukutane tukiwa wenye afya njema.Binafsi namshukuru kwa mapenzi yake kwangu kwani wapo wenzetu wanasumbuliwa na maradhi na matatizo lukuki ikiwemo misiba.
Shoga yangu, baada ya wiki iliyopita kuelezea namna ya kucheza na maeneo flani ya waume zetu ili kuwapa mushawasha wa mahaba nao kutuburudisha, leo nitazungumza nawe kuhusu madhara ya kumpa mumeo chakula cha usiku gizani.
Nimeamua kuliongelea suala hili kwa sababu wapo wenzetu wanapokula chakula cha usiku huzima taa, wanashangaza kwa kweli!Shoga yangu, kabla sijasonga mbele hebu nikuulize, hivi unapompa mumeo chakula cha usiku kwenye giza unamuogopa, unaona aibu au inakuwaje?
Sasa shoga yangu mwenye tabia hiyo ngoja leo nikuambie ukweli kwamba ukitaka kufurahia chakula cha usiku kiliwe kwenye mwanga wa kutosha.Raha ni pale utakapokuwa na mumeo mnakula chakula hicho kila mmoja wenu avione viungo vyote vya mwenzake.
Kitendo cha mumeo kuiona midomo, macho yako na maeneo mengi ya mwili wako kitamfanya afurahie chakula chako na kupata hamasa ya kupenda kula nawe kila siku.
“Siyo siri mke wangu, kama siku zote ungekuwa unanipa chakula cha usiku kwenye mwanga wa kutosha kama leo, ningenenepaje?” mumeo hata kama hana tabia ya kukusifia atafunguka tu.
Halikadhalika, hata wewe kitendo cha kuona midomo ya mumeo inavyocheza na macho yake yakiwa hayabanduki usoni kwako na kama mumeo mtundu, wakati huo wa chakula cha usiku atakukonyeza, hakika utajisikia raha ya kupitiliza.
Mtu asikudanganye shoga yangu, hakuna kitu kitamu kama kula chakula cha usiku kwenye mwanga wa kutosha kwani kila mmoja atajiachia atakavyo kwa mwenzake.
Shoga, unapozima taa wakati wa chakula cha usiku unahatarisha ndoa yako, na kwa nini ufanye hivyo wakati uliyemuandalia chakula hicho ni mumeo uliyeahidi kujitoa kwake kwa kila kitu? Kama wewe ni miongoni mwa wanaofanya hivyo hebu leo usiku kula na mumeo chakula cha usiku kwenye mwanga wa kutosha.
Wakati mnakishambulia chakula hicho usiwe na papara, naamini atakushika hata kwenye maeneo ambayo alikuwa hayagusi kabisa nawe utafurahia kuwa naye na kujiona ulikuwa unakosa vitu adimu maishani mwako. Bye!
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI

AMANDA AZIDIWA, ASHINDWA KUMZIKA MEZ B


MREMBO kunako tasnia ya filamu Bongo, Tamrina Mohamed Poshi ‘Amanda’ ameshindwa kuhudhuria mazishi ya aliyekuwa mwanamuziki wa Bongo Fleva, Moses Bushagama aliyefariki mwishoni mwa wiki iliyopita mkoani Dodoma kutokana na kuugua ghafla.
Mrembo kunako tasnia ya filamu Bongo, Tamrina Mohamed Poshi ‘Amanda’.
Akizungumza na Uwazi kwa masikitiko, Amanda ambaye pia ni mtu wa karibu na marehemu, alisema kuwa alishapanga kusafiri kwenda Dodoma kwa ajili ya maziko lakini kitendo cha kuugua ghafla kimeharibu kila kitu.
“Imeniuma sana kwa sababu ya ugonjwa wa taifodi kuniandama ambapo nilikuwa nikitapika mfululizo,” alisema Amanda.Mez B alikuwa akiumwa ugonjwa wa homa ya mapafu, alikuwa amelazwa katika Hospitali ya Mwananchi kabla ya umauti kumkuta. Amezikwa Jumatatu katika makaburi ya Wahanga mkoani Dodoma.
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI

JOYCE KIRIA ADAIWA MILLION 500


MTANGAZAJI wa Kipindi cha Wanawake Live, Joyce Kiria amepokea samansi ya mashtaka kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la Dimani, Zanzibar, Abdallah Sharia Ameir (CCM) ambaye amedai amlipe fidia ya kumdhalilisha sh. Milioni 500 au amuombe radhi kupitia  kipindi chake.
 
Mtangazaji wa Kipindi cha Wanawake Live, Joyce Kiria.
Akiongea na Uwazi, Joyce Kiria alisema kuwa amepokea barua hiyo kwa mikono miwili na anawasubiri wanasheria wake ili waijadili.“Nilimpokea mke wa Mbunge aitwaye Hawa kama mwanamke mwenye matatizo ambaye alifika kutoa sauti yake ili watu wamsaidie mtoto wake mwenye ulemavu.
Baada ya kuongea naye nilimtafuta mheshimiwa ili kumpa nafasi naye aongee ya kwake kama wajibu wangu, lakini cha kushangaza yeye alinikamata na kunipeleka polisi, leo anasema nimemdhalilisha,” alisema Joyce .
Joyce anadaiwa fidia na Mbunge huyo kwa kuitangaza habari ya kumtelekeza mtoto mlemavu ambaye alilepelekwa kwenye kipindi chake na mkewe, Hawa Deusi.
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI
© Copyright BONGO HABARI
Back To Top