Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

KWAKO Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima. Pole sana kwa masaibu yaliyokupata na bila shaka, Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema, atakujaalia afya njema hivi karibuni.
Binafsi mimi mwananchi wa kawaida  nisiyekuwa na cheo chochote cha dini wala siasa, ni mzima wa afya na ninaendelea na shughuli zangu za kila siku likiwemo hili la kukuandikia wewe barua.
Kama ulikuwa hufahamu, kupitia hii barua yangu huwa nawakumbuka watu mbalimbali wenye majina katika jamii yetu. Leo nimekukumbuka wewe, japo naamini hatujawahi kuonana ana kwa ana lakini nautambua mchango wako kama kiongozi wa dini mwenye heshima kubwa kwa waumini wengi walio nyuma yako.
Wengi hawategemei kukuona katika jambo lolote ambalo litakuwa kinyume na matakwa ya Mungu. Mungu ni mpole na mnyenyekevu. Kwenye amri zake ametuzuia kufanya matendo maovu likiwemo la matusi.
Hapo ndipo kwenye msingi wa barua yangu. Kama msikilizaji mwingine, nilipata kusikia sauti yako ikimdhihaki kiongozi wa Kanisa Katoliki, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo kwa maneno machafu yasiyo na staha hata kidogo kutamkwa na kiongozi mkubwa wa dini kama wewe.
Nilijiuliza uliuweka uchungaji pembeni ulipokuwa unazungumza lugha kali kama ile? Maneno mazito kama yale hayakupaswa kuzungumzwa na mtu kama wewe, hata kama uliyekuwa unamtuhumu ametenda kosa kiasi gani, haikuwa busara hata kidogo kutamka maneno machafu yasiyo na hekima.
Maneno uliyoyatamka katika kinywa chako, yangetamkwa na mhuni wa mtaani wala nisingeshtuka. Nisingeona jambo hilo ni la ajabu kwani maneno kama hayo na mazito, yanatamkwa sana uswahilini kwetu.
Nimeshtuka sababu wewe ni mchunga kondoo wa Bwana. Wewe una dhamana ya kufundisha mema, ni kiongozi. Tena huongozi kikundi cha siasa, unaongoza kanisa lenye waumini wengi.Mbaya zaidi, kiongozi uliyemtusi naye ni kiongozi mkubwa wa dini. Ana dhamana kubwa ya kuwaongoza waumini kama wako au pengine zaidi yako.
Kimsingi busara zilipaswa kukuongoza kufikisha ujumbe uliokuwa umekusudia.
Kama uliona amekosea kutofautiana na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Baraza la Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (CPCT) na Jumuiya ya Kikristo (CCT) katika suala la Katiba Inayopendekezwa, ungetumia lugha nzuri kumueleza kwa hoja.

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright BONGO HABARI
Back To Top