Featured

    Featured Posts

    Social Icons

Loading...

AIBU KUBWA MREMBO ADAKWA KWA WIZI HOSPITALI!

 
MREMBO mmoja aliyejulikana kwa jina la Mariam Moshi (23), mkazi wa Mwananyamala Ujiji, aliponea chupuchupu kuuawa na wagonjwa wenye hasira kali waliolazwa katika Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar baada ya kudaiwa kuiba nguo. 
Mariam Moshi akihamaki baada ya kukamatwa na nguo anazodaiwa kuiba katika wodi ya wazazi Hospitalini Mwananyamala.
Walinzi wa hospitali hiyo walimuokoa mrembo huyo kwa kumnasua mikononi mwa wagonjwa hasa wajawazito walioenda kujifungua, waliodai kwamba Mariam aliingia katika wodi yao na kuwaibia.Tukio hilo lilitokea Machi 27, mwaka huu saa tisa alasiri, ambapo mama mmoja ndiye alishtuka kwa kuona amechukuliwa kitenge chake kipya.
Mama huyo alipobaini ameibiwa, alitoka nje na kuangaza macho huku na kule akiangalia alipoelekea Mariam aliyekuwa wodini kwao, ndipo alipomuona akiwa anatoka nje kulielekea geti ambapo aliwapigia kelele walinzi ili wamzuie.
 
Mariam akiwa mikononi mwa mlinzi wa hospitali hiyo.
“Walinzi walimsimamisha na kumuuliza kama aliiba kitu chochote wodini akirudishe, lakini alikataa katakata kuhusika ma wizi huo,” kilisema chanzo.
Hata hivyo, walinzi walipompekua, aligundulika kuwa na vitu alivyovifunga na kufunika kwa dera (gauni kubwa, refu alilokuwa amevaa).Askari wa kike walipomfunua gauni hilo, walimkuta akiwa na taulo ambalo alikuwa amelifunga kiunoni pamoja na kitenge alichokuwa akituhumiwa kukiiba wodini.
Baada ya wagonjwa kuona mali alizoiba mrembo huyo, ndipo akina mama wengine wakiwa na watoto wao walitoka wodini na kuanza kupiga makelele kwa hasira wakitaka apewe mkong’oto.
 
Walinzi hao wakitoa baadhi ya vitu alivyoiba.
Hata hivyo, walinzi wa hospitali hiyo walipoona Mariam amezongwa, ilibidi watumie nguvu kumuokoa na kumweka chini ya ulinzi wakisubiri namna ya kumpeleka polisi.Mariam alipohojiwa na waandishi wetu juu ya kitu kilichompeleka hospitalini hapo, alisema alikwenda kuwaona wagonjwa ambao hata hivyo alishindwa kuwataja. Alisema yeye ni mwenyeji wa Dodoma anayeishi Dar kwa kujitegemea.
Aliomba msamaha kwa kitendo alichokifanya, akisema kinatokana na maisha magumu na katika hali ya kushangaza zaidi, alipoulizwa kuhusu taulo alilokuwa amejifunga ndani ya dera alilovaa, alisema halikuwa la hospitalini hapo, bali aliliiba katika gesti aliyokuwa amelala siku hiyo.
 
...Wakimuhoji.
Wauguzi wa hospitali hiyo walidai malalamiko ya wagonjwa kuibiwa mali zao hospitalini hapo ni jambo la kawaida, hivyo siku hiyo ilikuwa ni ‘40’ ya Mariam.

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright BONGO HABARI
Back To Top