
MREMBO kunako tasnia ya filamu Bongo, Tamrina Mohamed Poshi ‘Amanda’ ameshindwa kuhudhuria mazishi ya aliyekuwa mwanamuziki wa Bongo Fleva, Moses Bushagama aliyefariki mwishoni mwa wiki iliyopita mkoani Dodoma kutokana na kuugua ghafla.
“Imeniuma sana kwa sababu ya ugonjwa wa taifodi kuniandama ambapo nilikuwa nikitapika mfululizo,” alisema Amanda.Mez B alikuwa akiumwa ugonjwa wa homa ya mapafu, alikuwa amelazwa katika Hospitali ya Mwananchi kabla ya umauti kumkuta. Amezikwa Jumatatu katika makaburi ya Wahanga mkoani Dodoma.
USISITE KUTUACHIA UJUMBE WAKO HAPO CHINI
Post a Comment